• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

29 WAHITIMU mafunzo ya waongoza watalii Namtumbo

Imewekwa kuanzia tarehe: December 21st, 2022

WAZAZI na walezi katika wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma wametakiwa kuchangamkia fursa ya uwepo wa chuo cha mafunzo ya maliasili kwa Jamii(CBCTC)Likuyu Sekamaganga wilayani humo kwa ajili ya kuwasomesha vijana wao ili waweze kupata ajira ya kuongoza wageni na watalii baada ya kuhitimu masomo yao.

Rai hiyo ilitolewa hivi karibuni na mwakilishi wa katibu mkuu wa wizara ya maliasili na utalii Dkt.Julius Ningu ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Namtumbo wakati alipokuwa akizungumza kwenye mahafali ya pili ya Astashahada ya waongoza watalii 29 chuoni hapo.

Ningu alisema kuwa kutokana na jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan kuifungua Tanzania katika masuala ya utalii,wazazi wanapaswa kukitumia chuo hicho kwa ajili ya kusomesha vijana wao ili hapo baadae waweze kujiajiri na kupunguza wimbi la kuzagaa ovyo mitaani bila kazi.

Akizungumza katika mahafali hayo,Ningu amewataka wahitimu hao kujenga utamaduni wa  kuwa na tabia ukarimu,uadilifu na uaminifu pindi watakapokuwa wanawaongoza wageni na watalii wanakuja mkoani Ruvuma na Nchini kwa ujumla kwa lengo la kutembelea vivutio mbalimbali.

Aidha amewahasa wahitimu hao kuwa na moyo wa uzalendo katika kutunza maliasili za taifa ambazo zimekuwa zikitoweka na kuharibiwa ovyo na majangili pamoja na watu wanaoendesha shughuli za kibinadamu kwenye hifadhi za wanyama pori.

Naye mwakilishi wa mkurugenzi wa Idara ya wanyamapori Nassoro Wawa ambaye pia ni Afisa wanyamapori mkuu alisema kuwa kuongezeka kwa idadi ya watu kumechangia kwa kiasi kikubwa kufanya shughuli za kibinadamu zikiwemo kujenga,kufanya kilimo na ufugaji kwenye hifadhi za wanyamapori ambapo amewataka wanaoendesha vitendo hivyo kuacha mara moja.

Francisca Malembeka akiongea kwa niaba ya mkurugenzi wa kitengo cha utafiti na mafunzo alisema kuwa  mwingiliano wa shughuli za kibinadamu kwenye mapito ya wanyamapori kumechangia uharibifu na kuleta migogoro hivyo amewataka kucha kufanya shughuli hizo na kwamba amewataka wahitimu hao kusaidia kulinda maliasili hizo pamoja na kujisomea vitabu mbalimbali kwa lengo la kuongeza ujuzi na kukaa na wazee kwa ajili ya kujua historia ya mababu wa zamani.

Kwa upande wake mkuu wa chuo hicho Jane Nyau alisema kuwa chuo chake tangu kuanzishwa kwake kimeweza kupata mafanikio mbalimbali ikiwemo kutoa mafunzo  kwa wananchi zaidi ya 5000,kuboresha maktaba,kuongeza udahili wa wanafunzi pamoja na kuboresha mabweni.

Nyau alisema kuwa mbali na mafanikio hayo lakini chuo kinakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo upungufu wa nyumba za watumishi,uchakavu wa majengo,upungufu wa mabweni,upungufu wa wakufunzi na ukosefu wa mtuza kumbukumbu.

Akisoma taarifa kwa niaba ya wahitimu wenzake,Abdul Mgwasa alisema kuwa elimu waliyoipata wataitumia katika kulinda maliasili za taifa na kuwa mabalozi wazuri wa kukitangaza chuo hicho popote waendapo.

Hata hivyo Mgwasa alisema kuwa katika kipindi chote walichokuwepo chuoni hapo wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa umeme,mahema,mabweni,ukosefu wa viona mbali pamoja na ajira ya waongoza watalii.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.