• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

AGRA yazindua mkakati wa kukuza masoko ya kilimo

Imewekwa kuanzia tarehe: July 13th, 2023

Mpango mkakati wa AGRA wenye kaulimbiu ya kuchochea masoko jumuishi na yenye ushindani katika kilimo ili kuleta mabadiliko kwenye mifumo ya chakula nchini Tanzania umezinduliwa mjini Dodoma leo Jumatano.

Uzinduzi huo umefanywa  Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Hamis Ulega ambaye alkipongeza AGRA kwa kuja na mkakati huo wenye kugusa maeneo man manne muhimu.

Katika uzinduzi huo alikuwepo pia Waziri Mkuu Mstaafu na Mwenyekiti wa Baraza la Rais la chakula na kilimo, Mizengo Pinda.

Katika salmu zake kwenye uzinduzi huo Waziri wa Kilimo, Hussein Mohamed Bashe, akiwakilishwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Gerald Geofrey Mweli alisema serikali imeweka kipaumbele katika sekta ya kilimo ili kutengeneza maisha zaidi huku ikihakikisha kuwa vijana na wanawake wanajumuishwa.

“Tanzania inalenga kuwa ghala la chakula kwa Afrika na dunia nzima. Tumejitolea kufungua uwezo wa sekta ya kilimo, ambayo kwa sasa inachangia asilimia 25 ya Pato la Taifa na ni chanzo kikuu cha fedha za kigeni na chanzo cha ajira na utajiri.”

Alisema pamoja na mabadiliko ya teknolojia pia rais sanmia suluhu Hassan ametoa kibali cha kuajiri maofsia ugani wa kutosha na vifaa kusaidia kuleta mapinduzi

Pinda akizungumza alisema pamoja na kutambua mafanikio makubwa ambayo Tanzania imefikia bado kuna kazi kubwa ya kukabili umaskini mkubwa uliopo vijijini.

Ametaka sekta zote na wizara husika kuendeleza juhudi za kupambana na umaskini wa kipato na kuipa mifumo ya chakula 

 "Tuna ardhi, tuna kila kitu kinachohitajika. Tunachohitaji kufanya ni kuweka kipaumbele katika maendeleo na uboreshaji wa mifumo ya chakula ili kujenga maisha endelevu na kuinua jamii za vijijini."

Pinda :.. Tumefanya vizuri katika maeneo mengi na kubwa ni utulivu wa nchi yetu...mfumo wetu wa chakula haujapewa nafasi ya kutosha..kufungua uelewa zaidi juu ya hali ya nchi na umuhimu wa kuongeza kasi ya kutumia ardhi yetu ipasavyo na ndani ya rdhi yetu ipasavyo na ndani ya kipindi kifupi." alisema Pinda.

Alisema kuna umuhimu wa Nidhamu ya kazi na kujikita katika teknolojia za kileo kama walivyo Israel ambao hawana mito lakini wana kilimo cha umwagiliaji chenye tija.

 

 

Mkakati huo umelenga kuwajengea uwezo vijana na wanawake wa Kitanzania katika mnyororo wa thamani wa kilimo na hivyo kukuza ajira ukuaji wa ustawi wa jamii na uchumi.

Mkakati huo unajumuisha uboreshaji wa upatikanaji wa fedha na masoko, na kukuza utumiaji wa teknolojia mahiri za hali ya hewa na matumizi ya pembejeo, kama vile mbegu na mbolea.

Mkakati huo umelenga kuwa na jukwaa thabiti la kushirikisha maarifa na ubunifu na kukuza mijadala yenye maarifa kuhusu changamoto katika kilimo na biashara na kuboresha ufikiaji wa afua muhimu za kifedha kwa lengo la kuwezesha matumizi makubwa ya teknolojia na sayansi katika kilimo.

Mkakati huo unatarajiwa kunufaisha wakulima milioni tatu nchini kwa kuwapatia masoko ya mazao yao. 

Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana katikauzinduzi huo Mkakati huo umeganyiwanyika katika maeneo tofauti Kijiografia ikiwamo Nyanda za Juu Magharibi, Kanda ya Kati, Nyanda za Juu Kusini, Nyanda za Juu Kaskazini na Zanzibar. 

Aidha imeelezwa kuwa mazao yaliyopewa kipaumbele ni pamoja na mahindi, mtama, maharagwe, mihogo, alizeti, soya, ngano, viazi na mazao ya bustani.

Akizungumza wakati wa hafla ya kuzindua mkakati huo, Mkuu wa Kikanda wa AGRA, Afrika Mashariki, Profesa Jean Jacques M. Muhinda   alisema taasisi yake katika miaka hiyo mitano imelenga kuunga mkono juhudi za serikali ya Tanzania kuwa na uzalishaji mkubwa wa chakula.

“Tanzania imeonyesha umahiri katika kubadilisha mifumo yake ya kilimo cha chakula. Katika kipindi cha miaka mitano ijayo, tunanuia kusaidia kufungua fursa zaidi za kilimo na masoko wakati nchi inapoendelea kufanya mabadiliko chanya kwenye kilimo. Tumejitolea kuunga mkono vipaumbele vya serikali kwa sekta ya kilimo  ambayo imekuwa ikijijenga kwa miaka mingi.”

AGRA ambayo iliingia Tanzania mwaka 2006 imekuwa ikifanya kazi na serikali na mashirika binafsi na yale ambayo si ya kiserikali katika kuvutia uwekezaji, kusaidia mageuzi ya sera na kutoa zana za kilimo, maarifa na msaada kwa wakulima.

Aidha AGRA imeshirikiana na sekta binafsi kupitia Tanzania Agro-Industrialization Development Flagship,TAIDF, katika kuhakikisha kilimo kinakua na kinachangia katika pato la Taifa.

TAIDF ni mradi mkubwa wa kuwezesha maendeleo ya viwanda vya kilimo kwa kuhamasisha na kuratibu ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi; katika mradi huu ufadhili wa Dola za Marekani milioni 300  zilipatikana na kunufaisha wakulima zaidi ya milioni moja. 

Serikali pia ilitoa vivutio mbalimbali vya kodi ili kuvutia uwekezaji kutoka sekta binafsi.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Gerald Geofrey Mweli alisema Tanzania imelenga kuwa ghala la chakula kwa nchi za Afrika na duniani kote na hivyo haina budi kufungua uwezo wa sekta ya kilimo.

“Tanzania inalenga kuwa ghala la chakula kwa Afrika na dunia nzima. Tumejitolea kufungua uwezo wa sekta ya kilimo, ambayo kwa sasa inachangia asilimia 25 ya Pato la Taifa na ni chanzo kikubwa cha fedha za kigeni na chanzo cha ajira na utajiri." alisema Mweli.

Mwei alisema kwamba serikali ya awamu ya sita imeweka kipaumbele sekta ya kilimo ili kukiwezesha kupaa huku ikisaidia kupata ajira wanawake na vijana.

Uzinduzi wa mkakati huo mpya wa AGRA unafanyika wakati Tanzania ikijiandaa kuwa mwenyeji wa Kongamano la Mifumo ya Chakula Afrika 2023 (AGRF) litakaloanza Septemba 4  na kumalizika Septemba  8  mkoani Dar es salaam.

AGRF ni jukwaa kuu la Afrika lenye lengo la kuendeleza ajenda ya kilimo na mifumo ya chakula.

Mkutano huo utaleta pamoja makundi mbalimbali ikiwamo viongozi, watunga sera, wanasayansi, wakuu wa serikali, taasisi za kibinafsi, wakulima na vijana: ambao watakubaliana juu ya hatua za kivitendo ili kupata suluhisho kwa mifumo ya chakula barani Afrika.

"Jukwaa la mwaka huu lina umuhimu wa kipekee katika safari ya bara la Afrika kuelekea usalama wa chakula na ustawi wa pamoja." alisema 

Mada ya mkutano wa 2023,itakuwa  Regenerate, Recover, Act: Africa’s solutions to Food Systems Transformation, inalenga kuhakikisha bara la Afrika linaonesha umadhubuti wake katika kubadilisha mifumo ya chakula ili kuzalisha chakula cha kutosha na chenye lishe ndani yake na kuboresha jinsi kinavyozalishwa hasa ukizingatia mabadiliko ya hali ya hewa.

Afrika kwa sasa ni muagizaji mkuu wa chakula kutoka nje, na inaonekana uagizaji wa chakula utaendelea kupanda kutoka dola bilioni 43 mwaka 2019 hadi dola bilioni 110 mwaka 2025 kama hatua za makusudi zisipochukuliwa kukabili hali hiyo.

Kwa mujibu wa tovuti ya AGRA, shirika hilo linafanya kazi zake kuwiana na Mpango wa Kuendeleza Sekta ya Kilimo nchini (ASDP II), unaolenga kubadilisha mifumo ya kilimo nchini Tanzania sambamba na kuongeza tija na kipato kwa wakulima wadogo.

AGRA pia inachochea ushirikishwaji wa sekta binafsi na uwekezaji katika kilimo kwa kushirikiana na serikali na washirika wa kimkakati. 

Baada ya kujenga msingi thabiti wa teknolojia, ubia na miundo, AGRA iko tayari kuongeza kilimo chenye jumuishi na chenye ushindani nchini Tanzania.

Mkakati wake wa 2017-2021 uliunganisha ulilenga kuchochea na kudumisha Mabadiliko ya Kilimo Jumuishi. Mabadiliko hayo yalilenga kuongeza mapato na kuboresha usalama wa chakula kwa kaya za wakulima wadogo milioni 1.5 kwa kuwekeza dola za Marekani milioni 28.

kiasi hicho cha  fedha kimewekezwa  ambapo dola milioni 11.3 zilisambazwa kupitia ruzuku 31 tofauti ambapo wakulima 742,865 walinufaika.

Aidha, Mpango wa Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili umenufaika na ruzuku kubwa ya dola milioni 1.672. Zaidi ya wakulima 42,000 wamefaidika moja kwa moja na mpango huo, wakiongezewa na wakulima 34,000 walioathiriwa kupitia mipango mingine mbalimbali.

Kutokana na juhudi hizo Mauzo ya mazao chini ya mipango ya AGRA yalivutia $1.6 milioni.

Wakati AGRA ikizindua mpango mkakati wake mpya, shirika limedhamiria kuendelea kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kuleta mabadiliko na ukuaji wa sekta ya kilimo nchini Tanzania.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.