• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

AINA mpya ya utalii Tanzania inavyopendwa Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: July 3rd, 2024

KUELEKEA tamasha kubwa la kitaifa  la utalii wa kiutamaduni ambalo linatakiwa kufanyika mkoani Ruvuma kuanzia Julai 20 hadi 27 mwaka huu,ni vema kufahamu  zao jipya la utalii ambalo limekuwa linafanyika katika nchi zinazoendelea na sasa linafanyika mkoani Ruvuma.

Zao hilo la utalii hapa nchini ambalo kwa mara ya kwanza limefanyika mkoani Ruvuma ni utalii wa kuelea na mitumbwi katika Mto Ruvuma wenye urefu wa Zaidi ya kilometa 800.

Mwaka huu watalii wengine wamefanya utalii wa kuelea na mitumbwi  katika Mto Ruvuma,kupiga kasia  umbali wa Kilometa 70 kutoka Mpelo wilayani Mbinga hadi katika Pori la Akiba la Liparamba wilayani Nyasa.

Wageni hao wakiwa wanateleza na mitumbwi katika mto huo walishuhudia mandhari za kuvutia na Wanyama mbalimbali wakiwemo mamba,tembo na viboko huku macho ya Wanyama hao wakiangalia mitumbwi ya wageni hao.

Agosti 2019 Mkoa wa Ruvuma kwa mara ya kwanza ulipokea watalii  22 wa   kihistoria kutoka barani Ulaya na Marekani ambao wamefanya utalii wa kwanza Tanzania wa kuteleza katika Mto Ruvuma  kwa kutumia mitumbwi.

Utalii wa namna hii umekuwa unafanyika katika nchi Afrika ya kusini ambapo kwa Tanzania hii ni mara ya kwanza kupata watalii wanaoteleza kwenye mito, kwa kuwa watalii wanaofika hapa nchini wamekuwa wanatembelea mbuga za wanyama, kupanda milima na maeneo mengine.

Watalii hao walitumia siku kumi kuteleza katika mto Ruvuma umbali wa kilometa 160, kupitia msitu wa Hifadhi wa Taifa wa mazingira asilia wa Mwambesi ambapo kila siku waliteleza kilometa 16 na kuweka kambi  katika vijiji vilivyopo kando ya mto huo.

Watalii hao walitumia mitumbwi ya kawaida ya kupiga makasia ambayo imetengenezwa mkoani Arusha na kwamba watalii hao wamemaliza utalii wao kwa usalama.

Watalii waliongozwa na wenyeji ambao wanayajua vizuri maeneo ya mto Ruvuma ambao una miamba, vilima na maporomoko.

Mkoa wa Ruvuma, umeufungua Mto Ruvuma kama chanzo kingine cha utalii Tanzania, cha watalii kufanya utelezi katika mto,huu ni utalii ambao unagharama kubwa na unapatikana katika nchi zilizoendelea duniani.

Wilaya ya Tunduru Septemba 2019 ilipokea watalii wengine 50 kutoka ulaya.Hivi sasa Tunduru imefunguliwa na kupelekwa duniani ambapo Wilaya ya Tunduru ina vivutio vingi vya utalii vikiwemo mbuga za wanyama, ndege na mimea adimu duniani.

Watalii waliotembelea Tunduru wamekabidhiwa nakala ya muongozo wa vivutio vya utalii na uwekezaji katika Mkoa wa Ruvuma ambao ulizinduliwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa siku ya kongamano la uwekezaji katika Mkoa wa Ruvuma mwaka 2019.

Safari hiyo ya aina yake ya watalii kutoka Ulaya,licha ya kupata mafanikio makubwa imesaidia kutambua changamoto zikiwemo miundombinu hafifu ya barabara kufikia baadhi ya maeneo kama Msitu wa Taifa wa asili wa Mwambesi.

Watalii hao mara baada ya kumaliza safari yao, wameahidi wanavyorudi katika nchi zao,wanakwenda kutafuta watalii wengine ambao watakuja kuteleza katika Mto Ruvuma.

“Safari yetu ya siku kumi kusafiri katika Mto Ruvuma imethibitisha kuwa Mkoa wa Ruvuma una utajiri wa vivutio vya kipekee vya utalii kama Mto Ruvuma, tunavyorudi nyumbani tunakwenda kupeleka habari hizi kwa wenzetu, hivyo mtarajie kupokea wageni wengi zaidi’’, anasisitiza Dkt. Menagon.

Manyise Mpokigwa ni Meneja Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Kanda ya Kusini ambao wameratibu ujio wa watalii kutalii katika Mto Ruvuma na Msitu wa Hifadhi wa Taifa wa mazingira asilia Mwambesi wilayani Tunduru, anasema tukio hilo limesaidia kuvitangaza  vivutio vilivyopo kusini.

 Amesema watalii hao wameongeza pato la Taifa kwa serikali na kwa jamii kwa   sababu wakiwa katika vijiji kando kando mwa Mto Ruvuma waliweza kununua bidhaa  za  wananchi.

Hata hivyo amesema TFS kwa kushirikiana na serikali kuu inaendelea kuboresha miundombinu ya  barabara katika misitu hiyo ili watalii wanapoingia kufanya utafiti na utalii waweze kupita kwa urahisi na kuvutia idadi kubwa ya wageni wa ndani na  nje ya nchi.

Mto Ruvuma wenye urefu wa kilometa zaidi ya 800 umeanzia Songea mjini kwenye milima ya Matogoro, na kupita katika wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma kisha kuendelea     katika baadhi ya wilaya za Mkoa wa Mtwara na kumwaga maji yake Bahari ya Hindi.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.