• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

ASILIMIA 90 ya vitabu vya Tanzania havina maudhui ya ukweli kuhusu uhuru wa Tanzania

Imewekwa kuanzia tarehe: August 17th, 2020

Asilimia 90 ya vitabu vya Tanzania  havina maudhui ya ukweli kuhusu Uhuru wa Tanzania

Waziri wa Habari, Utamaduni, sanaa na Michezo,  Dkt Harrison Mwakyembe amesema asilimia 90 ya vitabu vya Tanzania havina maudhui ya ukweli kuhusu Tanzania ilivyopata uhuru wake bila kumwaga damu .

Waziri Mwakwembe ameyasema hayo wakati alipotembelea Makumbusho ya Taifa ya  Majimaji Mjini songea hivi karibuni katika ziara yake aliyoifanya mkoani Ruvuma ya kutembelea maeneo ya  harakati za ukombozi dhidi ya wakoloni.

Amesema suala la kupata uhuru ni mchakato ,hivyo uhuru wa Tanzania haujapatikana kwa njia ambazo waandishi wa vitabu  wamezitaja  kwa sababu kuna wananchi walijitolea katika harakati za ukombozi hadi kumwaga damu.

Dkt.Mwakyembe akiwa katika Makumbusho ya Taifa ya Majimaji alishuhudia historia ya ukombozi iliyoanza wakati wa Vita vya Majimaji iliyofanyika mwaka 1905 hadi 1907  ambapo katika vita hivyo mashujaa 67 walivyongwa na kuzikwa kwenye makaburi yaliyopo ndani ya makumbusho hayo..

Kulingana na Mwakyembe,vitabu vingi vya Historia ya Upatikanaji wa Uhuru ya Tanzania inaonesha kuwa Tanzania bara ilipata Uhuru bila kumwaga damu jambo ambalo amesema sio sahihi kwa sababu tangu miaka ya Vita vya Majimaji Wananchi wa Tanganyika waliukataa Utawala wa Wajerumani ambao walikuwa wanaitawala Tanzania wakati ule ambapo baadhi yao walipoteza maisha kwa kumwaga damu.

“Mababu zetu walipigania uhuru kwa kumwaga damu kwa lengo la kupinga Utawala wa Wajerumani na ndipo walipoanzisha vita ya Majimaji na kupigana tangu mwaka 1905 hadi 1907 na ndipo mashujaa wa vita vya majimaji 67 walinyongwa na kuzikwa katika kaburi la pamoja’’,alisisitiza.

Hata hivyo amesema vitabu vingi historia havionyeshi Tanzania ilipata Uhuru kwa Kumwaga damu,badala yake vitabu vinaonesha Tanzania ilipata Uhuru bila kumwaga Damu jambo ambalo Waziri Mwakyembe amesema  hakubaliani na waandishi wa Historia ya Tanzania.

“Kwa kweli hapo sikubaliani na waandishi wa Historia ya Tanzania nafikiri waanzie mwanzo kabisa badala ya kuanzia  wakati wa Uhuru’’,alisisitiza Dkt.Mwakyembe.

Dkt.Mwakyembe ameagiza kutunzwa kwa makaburi ya Mashujaa  67 waliozikwa katika Kaburi moja ndani ya Makumbusho ya Majimaji na kwamba mashujaa hayo walipinga Utawala wa Wajerumani.

Amesema wakoloni walikuwa wanyonyaji ambao  waliwatumikisha wananchi kwa ujira mdogo na kulipa kodi  kwa manufaa ya Utawala wa Ujerumani.

 Waziri Mwakyembe ameshauri  waandishi wa vitabu vya historia waanzie toka enzi za vita ya Majimaji vilivyopigana katika Mikoa nane ya Tanzania ukiwemo Mkoa wa Ruvuma na kuonesha idadi ya mashujaa waliomwaga damu.

Pia Mwakyembe ameshauri Wanafunzi kwenda kujifunza uhalisia wa vitendo,picha mbalimbali na vifaa halisi vilivyotumika katika vita ya Majimaji kwenye Makumbusho ya Taifa ya Majimaji.

Imeandikwa na Netho Credo na Jackline Clavery

Maafisa Habari Serikalini

Agosti 17,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.