• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

ASILIMIA 97 za huduma za kibingwa za Ulaya na India sasa zinapatikana nchini

Imewekwa kuanzia tarehe: August 26th, 2024

Na Gustaph Swai-RS Ruvuma

Naibu Waziri wa Afya, Mheshimiwa Dr. Godwin Mollel, ameeleza mafanikio makubwa yaliyofikiwa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika sekta ya afya.
Akizungumza wakati wa ibada ya kumsimika Abate mpya wa Peramiho iliyofanyika katika Kanisa la Peramiho, Dr. Mollel amesema kuwa kwa asilimia 97, serikali imewezesha huduma za kiteknolojia za afya zinazotolewa Ulaya na India  kupatikana  katika hospitali zilizopo hapa nchini.


"Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye sekta ya afya amefanya uwekezaji mkubwa, ameshakamilisha asilimia 97 ya teknolojia tuliyokuwa tunaifuata Ulaya na India tayari iko kwenye nchi yetu," alieleza Dr. Mollel

Naibu waziri ameitaja teknolojia hiyo kuwa na uwezo wa kurahisisha huduma za upasuaji kama vile uvimbe chini ya sakafu ya ubongo, kifua, moyo, mgongo, na huduma kwa watoto wanaozaliwa na seli mundu ambapo huduma zote hizo sasa zinatolewa nchini.


Sanjari na hayo Naibu Waziri ameeleza umuhimu wa lishe bora katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini, ambayo inaongoza kwa uzalishaji wa chakula lakini inakabiliwa na tatizo la lishe na udumavu.


Ametoa wito kwa viongozi wa dini kuwasaidia wananchi kutambua umuhimu wa lishe bora ili kuimarisha afya ya jamii na kuweza kuchangia maendeleo katika Taifa.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Songea Mheshimiwa Kapenjama Ndile  ameitaja hospitali ya Rufaa ya Peramiho inayoongoza katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini na Kusini kwa kuhudumia wagonjwa wengi wa figo kwa wakati mmoja.

Katika juhudi za kuunga mkono sekta ya afya, Naibu Waziri wa Afya ameeleza kuwa serikali imedhamria kuondoa vikwazo kwa wawekezaji wanaotaka kuwekeza katika sekta ya afya nchini, hususan katika masuala ya kodi.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.