• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

ASKOFU Tunduru awaasa wazazi kuwa mfano katika maadili mema

Imewekwa kuanzia tarehe: July 9th, 2023

WAZAZI na walezi nchini,wametakiwa kujenga tabia ya kuzungumza na kuwa karibu na watoto wao mara kwa mara,jambo litakalosaidia kupungua kwa vitendo viovu ikiwemo ukiukaji wa maadili  ,matumizi ya dawa za kulevya na unyanyasaji wa kijinsia

Wito huo umetolewa na Mhashamu Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Tunduru-Masasi Mhasham Filbert Mhasi,katika mahubiri yake kwenye  Jubilei ya  kutimiza miaka 25 kwa mapadri watatu  na miaka 40 ya padri mmoja iliyofanyika katika Kanisa Katoriki Tunduru mjini.

Alisema suala la malezi ya watoto siyo  jukumu la viongozi wa kanisa au serikali ,bali kila mmoja katika jamii inawajibu huo ili kupata kizazi salama kitakachoishi kwa kufuata maadili ya Kitanzania na kuzingatia mafundisho ya  Mwenyezi Mungu.

Askofu Mhasi ameitaka jamii kukemea mambo mabaya,kuwafundisha watoto wao maadili mema  na kuhakikisha wanawapa elimu  itakayowasaidia kukabiliana na changamoto za maisha.

“wazazi na walezi  tunatakiwa kuzingatia namna gani tunakuwa pamoja na vijana wetu tangu wakiwa watoto, vijana wetu wanahitaji mwongozo wa karibu,tunapowaacha wanatafuta mwongozo  sehemu nyingine ikiwemo kwenye mitandao wakifikiri kwamba inawasaidia,kumbe wanaingia kwenye mambo yanayoharibu safari ya maisha yao”alisema.

Aidha,amewaasa watoto na vijana kuwasikiliza wazazi  na walezi wao na kuwa karibu nao wakati wote  kwa kuwa wazazi wana mambo mema  na hawategemei kusikia wala kupata mambo mabaya kutoka kwa watoto wao.

Amewaomba wazazi kupinga kwa nguvu zote mila na desturi zenye madhara zinazochochea na kusababisha kumomonyoka kwa maadili kwa vijana hapa nchini.

Askofu Mhasi,amewataka waumini wa kanisa hilo kuendeleza upendo na mshikamano wao kwa wao na kwa viongozi wao, badala ya kunyoosheana vidole na kushutumiana katika mambo  yasiyokuwa na afya kwa kanisa.

Pia,amewataka viongozi wa Dini wakiwemo mapadri na watawa kuendelea kuwa mfano bora na kuhubiri matendo mema ili kuwasaidia waumini wao na jamii kwa ujumla kumjua Mungu wakati wote.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Tunduru Julius Mtatiro,amewapongeza mapadri hao kwa kutimiza miaka 25 na 40 ya utumishi wa kanisa na kueleza kuwa huoni wito mkubwa kuliko yote hapa Duniani.

Mtatiro,ameikumbusha jamii kuacha kupigana majungu na kuchukiana badala yake kuishi kwa upendo na unyenyekevu na kujiepusha na vitendo vinavyokwenda kinyume na maagizo ya Mungu.

Amewakumbusha wana ndoa umuhimu wa kupendana na kuishi kwa amani wakati wote ili  kujenga kizazi bora, chenye maadili mema,uaminifu,uadilifu na kinachomjua Mwenyezi Mungu.

Akizungumza kwa niaba ya mapadri wenzake Maiko Tesha alisema,kufika umri wa miaka 25 na 40 katika utumishi ni  mapenzi ya Mungu na kuwaomba waumini kuendelea kuwaombea ili waweze kudumu katika majukumu yao.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.