• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

Imewekwa kuanzia tarehe: June 1st, 2025

Taifa limeingia katika huzuni nzito baada ya kupokea taarifa za kifo cha mwanasiasa mkongwe na shujaa wa mapambano ya uhuru wa Tanganyika, Alhaj Mustafa Mohamed Songambele.

Mzee Songambele, ambaye alitimiza miaka 100 Jumapili iliyopita, amefariki dunia  jijini Dar es Salaam, ikiwa ni siku chache tu baada ya kusherehekea karne moja ya maisha yake.

Msiba upo nyumbani kwake Mwananyamala, huku maandalizi ya kuusafirisha mwili kuja Songea kwa ajili ya maziko yakiendelea.

Katika historia ya siasa za Tanzania, jina la Alhaj Songambele haliwezi kufutika. Alikuwa mmoja wa waanzilishi wa Chama cha TANU ,chama kilichoasisi harakati za kudai uhuru  akiwa miongoni mwa wanachama wa kwanza 30, na akapewa kadi namba 27.

Baada ya TANU na ASP kuungana na kuunda CCM, aliendelea kuwa mstari wa mbele katika ujenzi wa taifa.

Ni mtu aliyeshuhudia na kushiriki kwa vitendo historia ya ukombozi wa Tanganyika, akiwa bega kwa bega na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.

Safari ya uongozi ya Songambele ni sura ya pekee katika historia ya utawala wa nchi.

Aliweka rekodi ya kuwa Mkuu wa Wilaya wa kwanza nchini Tanganyika baada ya uhuru, akiteuliwa kuongoza Wilaya ya Pwani, ambayo leo ni sehemu ya Wilaya ya Ilala.

Hakuishia hapo aliteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, nafasi aliyopewa na Mwalimu Nyerere mwenyewe kutokana na uaminifu, weledi na uzalendo wake usiotetereka.

Alhaj Songambele hakuwa tu kiongozi wa siasa, bali pia mtu wa karibu sana na Mwalimu Nyerere.

Historia inamkumbuka kama mmoja wa wakazi wa Dar es Salaam waliompokea Mwalimu baada ya kuacha kazi ya ualimu ili kujitosa kikamilifu kwenye harakati za kudai uhuru.

Ndiyo aliyemsaidia Mwalimu kupata kiwanja cha kujenga nyumba Magomeni Mikumi  nyumba ambayo leo ni kumbukumbu hai ya maisha ya Baba wa Taifa, ikiwa makumbusho rasmi yanayohifadhi historia ya ukombozi wa taifa letu.

Kifo cha Alhaj Songambele si tu pengo kwa familia, bali ni pigo kubwa kwa historia ya Tanzania.. Mzee Songambele amepumzika, lakini historia yake itaendelea kuishi.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DKT Nchimbi awaongozawananchi kuuaga mwili wa Mzee Songambele

    June 02, 2025
  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.