• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

AWAMU ya pili uboreshaji daftari kuanza Ruvuma January 28

Imewekwa kuanzia tarehe: January 18th, 2025

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imezindua mafunzo kwa watendaji ngazi ya mkoa kuhusu Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya pili ambayo itajumuisha Halmashauri tatu za mkoa wa Ruvuma ambazo ni Tunduru DC, Namtumbo DC na Madaba DC.

Uzinduzi huo umefanyika katika ukumbi wa Chandamali mjini Songea mkoani Ruvuma, mgeni rasmi akiwa ni Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Mhe. Magdalena K. Rwebangira.

Mheshimiwa Rwebangira amewataka watendaji hao hasa wale waliowahi kufanya zoezi kama hilo kutumia uzoefu walionao na mafunzo wanayopatiwa kwa kufanya kazi zao kwa weledi, bidii na moyo wa kujituma ili kufanikisha zoezi hilo.

Ameongeza kuwa wakati wa Uboreshaji wa Daftari mawakala wa vyama vya siasa wataruhusiwa kuwepo katika vituo vya uandikishaji kwa kuwa ni muhimu na itasaidia kuleta uwazi katika zoezi zima na kutambua waombaji wa eneo husika hivyo kupunguza kutokea vurugu zisizo za lazima.

Naye Mratibu wa Uandikishaji Mkoa wa Ruvuma, Salumu Kateula, amebainisha kuwa awamu ya kwanza ya Uboreshaji wa Daftari ambayo ilianza tarehe 12 Januari inatarajia kukamilika Januari 18 ambayo imejumuisha Halmashauri tano katika mkoa linaendelea vizuri, na awamu ya pili ambayo itajumuisha Tunduru DC, Namtumbo DC na Madaba DC itaanza Januari 28 hadi Februari 3, 2025.

Amewasisitiza wananchi wa Halmashauri hizo kutumia muda huo kujitokeza kujiandikisha na kuboresha taarifa zao katika Daftari ili waweze kupata haki yao ya kupiga kura katika uchaguzi ujao.

Kwa upande wake Afisa Muandikishaji Jimbo la Madaba, Sajidu Mohammed, amesema wanaendelea kuwahamasisha wananchi kujitokeza kujiandikisha na kuboresha taarifa zao hasa makundi ya vijana waliotimiza umri wa miaka 18 na watu wenye ulemavu.

Kwa upande mwingine Afisa Muandikishaji Jimbo la Namtumbo, Juma Njelu, amesema anaamini wananchi watajitokeza kwa wingi kujiandikisha ili wapate vitambulisho kwa kuwa vimekuwa vikitumika kwa matumizi mbalimbali ikiwemo mikopo na dhamana.

Awamu ya kwanza ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura mkoani Ruvuma lilianza Januari 12 na linatarajiwa kukamilika Januari 18 katika Halmashauri tano ikiwemo Songea MC, Songea DC, Mbinga TC, Mbinga DC na Nyasa DC na awamu ya pili itaanza Januari 28 na kukamilika Februari 3 mwaka huu.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.