• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

BARABARA ya Mbinga-Mbambabay ilivyogeuka kivutio

Imewekwa kuanzia tarehe: April 20th, 2025

Wakati mwingine maendeleo hayaji kwa kelele, bali huingia kimya kimya na kuacha alama kubwa.

Hivi ndivyo ilivyotokea kwa barabara ya lami nzito yenye viwango vya kimataifa kutoka Mbinga hadi Mbambabay, mkoani Ruvuma ambayo sasa si tu kiungo muhimu cha usafirishaji, bali pia kivutio cha kipekee kinachowaacha wengi vinywa wazi.

Barabara hii yenye urefu wa zaidi ya kilomita 66, ambayo zamani ilikuwa changamoto kwa wasafiri na wakulima wa maeneo ya Nyasa, sasa imejengwa kwa kiwango cha lami na kugeuka kuwa njia ya kisasa inayoambatana na mandhari ya kuvutia ya milima, mabonde, kuelekea mwambao wa Ziwa Nyasa.


Barabara Inayochora Urembo wa Asili

Ukisafiri kutoka Mbinga kuelekea Mbambabay, ni kama unashuhudia picha halisi ya uzuri wa Tanzania Kusini. Milima ya Livingstone inavyopinda kwa ustadi, mabonde ya kijani kibichi yanavyojaa mazao, na upepo mwanana kutoka Ziwa Nyasa,haya yote hufanya safari isiwe ya kawaida.

“Ni barabara ambayo ukiipitia, huwezi kujizuia kushika simu yako na kupiga picha. Mandhari ni ya kipekee kabisa,” anasema Grace Mkisi, mjasiriamali wa utalii kutoka Songea.


Faida Zaidi ya Kusafiri

Mbali na kuvutia watalii, barabara hii imeleta mapinduzi ya kiuchumi kwa wakazi wa wilaya ya Nyasa. Wakulima sasa wanaweza kufikisha mazao yao sokoni kwa haraka,Pia, huduma za kijamii kama afya na elimu zimeboreshwa kwa sababu ya urahisi wa usafiri.

“Mgonjwa alikuwa akihitaji masaa matano hadi Mbinga Mjini, sasa ni saa moja tu,” anasema Daktari Modest kutoka Kituo cha Afya Mbambabay.

Hongera sana serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu kwa kuendelea kuifungua Wilaya ya Nyasa


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.