• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

BARAZA la madiwani Tunduru lapitisha makadirio ya bajeti mpya

Imewekwa kuanzia tarehe: February 16th, 2025

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru limekutana kujadili rasimu ya makadirio ya bajeti ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2025/26.

Rasimu ya Bajeti hiyo imepitishwa katika Baraza hilo la Madiwani kwa mwaka 2025/26 ni kiasi cha shilingi bilioni 47

Baraza hilo limeongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Mhe. Hairu Hemed Mussa, ambapo imewasilishwa na Afisa Mipango wa halmashauri hiyo, Bosco Mwingira kwa niaba ya Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri.

Mwingira amesema kuwa bajeti hiyo inalenga kuboresha miundombinu mbalimbali ikiwemo ya afya, elimu, kilimo, na sekta nyingine kwa maendeleo ya wilaya.

Madiwani wa kata ya Mchoteka na Kata ya Ligoma katika baraza hilo wameiomba serikali kushughulikia changamoto zinazowakabili wananchi wa kata zao, ikiwemo ukosefu wa huduma za afya, barabara na maendeleo ya kilimo.

Wamesema hali ya miundombinu katika kata zao inahitaji maboresho makubwa ili kuinua kipato na maisha ya wananchi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Chiza Cypirian Marando, alisema wanaendelea kukamilisha ujenzi wa Zahanati ya Mtangashari, ukarabati wa mabwawa ya samaki, pamoja na kuboresha kilimo cha umwagiliaji ili kuongeza uzalishaji wa mazao.

Aidha, Marando ameeleza kuwa Wilaya ya Tunduru imebarikiwa kuwa na rasilimali za madini aina ya shaba (copper) yanayopatikana katika Kata ya Mbesa ambayo pia yatasaidia kuongeza mapato ya halmashauri.

Mkurugenzi wa Halmashauri ameomba ushirikiano kutoka kwa madiwani na wananchi katika ukusanyaji wa mapato pamoja na kushirikiana katika ujenzi wa madarasa mapya katika Kata ya Ligoma ili kuboresha mazingira ya elimu kwa watoto wa wilaya hiyo.

Kwa upande wake, Makamu wa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ametoa mchango wake akisisitiza uboreshaji wa mapato ya ndani ya halmashauri.

Ameeleza kuwa ukamilishaji wa kilomita 1,206 za barabara unakadiriwa kuchukua takribani miaka nane, hivyo ni muhimu kuweka mkazo katika usimamizi wa fedha na rasilimali zilizopo.

Hata hivyo amesema kuwa bajeti ya fedha kuhusu ukarabati wa barabara kwa upande wao wameiachia Mamlaka ya Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini Tarura kushughulikia changamoto hizo.

Katika hitimisho la kikao hicho, madiwani walikubaliana kuwa asilimia 40 ya kiasi cha fedha zilizotengwa zitumike katika uboreshaji wa barabara ndani ya halmashauri.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.