• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

BILIONI 22 kuweka lami nzito barabara 20 za mji wa Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: June 6th, 2024

HALMASHAURI ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma ni miongoni mwa Halmashauri 12 nchini ambazo zimepata mradi wa uboreshaji wa miundombinu ya barabara za lami nzito ili kuboresha miundombinu ya miji,manispaa ya majiji.

Akitoa taarifa ya mradi huo kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas,Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Wakili Bashir Muhoja amesema katika Manispaa hiyo barabara za lami zenye urefu wa kilometa 10.1 zitajengwa ambapo jumla ya barabara 20 za katikati ya mji zitatengenezwa kupitia mradi huo.

Amesema Zaidi ya shilingi bilioni 22 zinatekeleza mradi huo ambao umefadhiliwa na Jumuiya ya Maendeleo ya Kimataifa (IDA) kupitia Benki ya Dunia ili kuboresha miundombonu na ushindani wa miji,manispaa na majiji nchini Tanzania.

Amebainisha kuwa mradi umeanza kutekelezwa ambapo hivi sasa mkandarasi amefikia asilimia 8.3 ya utekelezaji ujenzi wa barabara na ujenzi wa ofisi  ya TARURA umefikia asilimia 18 ambapo mradi unatarajia kukamilika Februari 2025.

“Tunaishukuru sana serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia mradi huo muhimu wa kuboresha miundombinu ya barabara za lami mjini Songea’’,alisema.

Akizungumza baada ya kukagua mradi huo ,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed ameishukuru serikali na wadau wengine wa maendeleo kwa kutenga fedha za kutekeleza mradi huo ambao unakwenda kuboresha barabara za lami za mji wa Songea.

Hata hivyo kutokana na mradi huo kuwa nyuma ya mkataba amemshauri Mkandarasi kuongeza nguvu kazi na vifaa ambapo ameyataja madhumuni ya miradi inayotekelezwa na serikali ni kuleta chachu ya maendeleo kwa wananchi hivyo kuchelewa kutekelezwa kwa miradi kuna punguza kasi chachu .

“Mkoa wa Ruvuma ni wazalishaji wakubwa wa chakula nchini ambacho kinapelekwa kwenye mikoa mingine na nje ya nchi,tungetarajia kuiona kasi ya ukuaji wa Mkoa inalingana na hali ya mambo inayoyafanya,watu wanatamani kuona utekelezaji wa shughuli za kijamii zinafanyika kwa kasi kubwa’’,alisisitiza Kanali Abbas.

Hata hivyo amesema hajafurahishwa na utekelezaji wa mradi huo kwa kiwango kilichofikiwa kwenye mradi huo hivyo ameagiza mradi huo utekelezwa kwa kasi ili wananchi waanze kunufaika na mradi huo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.