• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

BILIONI NNE kutekeleza mradi wa maji utakaonufaisha wakazi 60,868 Mbinga

Imewekwa kuanzia tarehe: April 16th, 2025

Wakazi zaidi ya 60,868 wa kata nane katika Halmashauri ya Mji Mbinga, mkoani Ruvuma, wanatarajia kuondokana na changamoto ya ukosefu wa maji safi na salama baada ya Serikali kutenga zaidi ya Shilingi bilioni 4.01 kwa ajili ya kuboresha huduma hiyo muhimu.

 Kati ya fedha hizo, Shilingi milioni 755.2 zitatumika kumlipa Mkandarasi Kampuni ya Ngogo Engineering Ltd itakayojenga mradi huo, huku zaidi ya Shilingi bilioni 3.25 zikienda kwa Kampuni ya Simba Pipe Industries Ltd kwa ajili ya kutengeneza na kusafirisha mabomba ya maji kutoka kiwandani hadi Wilaya ya Mbinga.

Akizungumza katika hafla ya utiaji saini mkataba wa mradi huo, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbinga Mjini (MBIUWASA), Mhandisi Yonas Ndomba, alisema mradi huo utahusisha ujenzi wa vyanzo viwili vya maji vyenye uwezo wa kuzalisha lita 1,613,200 kwa siku, matenki manne yenye ujazo wa lita 525,000 na mtandao wa bomba wa kilometa 57.

Amesema Mradi huu utakapokamilika, huduma ya maji katika kata za Ruhuwiko, Mbinga A, Betherehem, Matarawe, Lusonga, Masumuni, Mbinga Mjini B na Mbambi itapatikana kwa asilimia 97.8.

Hata hivyo amesema hivi sasa, mahitaji ya maji katika Mji wa Mbinga ni lita 5,478,000 kwa siku, wakati uzalishaji halisi ni wastani wa lita 3,797,000, sawa na asilimia 69 ya mahitaji, hivyo kuleta upungufu wa lita 1,681,000. Mhandisi Ndomba aliishukuru Serikali kupitia Wizara ya Maji kwa kutenga fedha hizo na kutoa kibali cha utekelezaji wa mradi huo, ambao unalenga kumaliza kabisa mgao wa maji kwa wakazi wa Mbinga.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Mbinga,Mheshimiwa  Kisare Makori, alisisitiza umuhimu wa utekelezaji wa mradi huo kufanyika kwa viwango vya juu na kwa wakati. Alizitaka kampuni husika kutoa ajira za muda kwa wananchi wanaoishi karibu na eneo la mradi, ili kuwawezesha kushiriki moja kwa moja kwenye uboreshaji wa huduma hiyo. 

Amesema kuwa mradi huo utawezesha mji wa Mbinga kufikia asilimia 98.3 ya upatikanaji wa maji safi, hatua inayozidi lengo la Ilani ya Uchaguzi ya CCM la asilimia 95 kwa maeneo ya mijini.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.