• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

CWT Songea yaipongeza serikali kwa kutatua changamoto za walimu

Imewekwa kuanzia tarehe: March 27th, 2025

Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Songea kimeipongeza Serikali ya awamu ya sita kwa kuhakikisha walimu wanapandishwa madaraja kwa wakati, wanapata daraja la mseleleko, na kulipwa viwango vipya vya mishahara.

 Katibu wa chama hicho, Neema Lwila, alitoa pongezi hizo jana wakati akisoma risala ya walimu kwenye Mkutano Mkuu wa CWT uliofanyika katika ukumbi wa Anglikana mjini Songea.

Lwila alisema changamoto ya walimu waliokuwa na ajira ya pamoja kuachana kimadaraja imepata suluhisho baada ya Serikali kushirikiana na CWT kupitia Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora. Aliongeza kuwa juhudi hizo zinaendelea ili kuhakikisha walimu wote wanapata haki zao kwa wakati.

Aidha, Lwila alimpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kujenga zaidi ya shule 600 za msingi na sekondari, kuboresha miundombinu, kuajiri walimu wapya, na kuanza kulipa madeni ya walimu. Hata hivyo, alisisitiza kuwa bado walimu wanadai fedha nyingi na akaiomba Serikali kuwabana wakurugenzi wa halmashauri kuhakikisha mapato ya ndani yanatumika kulipa madeni yasiyohusiana na mishahara.

Afisa Elimu Msingi wa Manispaa ya Songea, Hossen Mghema, aliwataka walimu kuwa wazalendo kwa chama na kuiunga mkono Serikali kwa kuwa imefanya maboresho makubwa katika sekta ya elimu. Alibainisha kuwa mazingira ya kufundishia yameboreshwa, nyumba za walimu zimejengwa, na vifaa vya kufundishia vimetolewa ili kusaidia utoaji wa elimu bora.

Mghema alihimiza walimu na wanafunzi kutunza miundombinu ya shule ili idumu kwa muda mrefu kwa kuwa Serikali inatumia fedha nyingi kuitekeleza. Alisema Serikali inaendelea kupandisha madaraja ya walimu na kulipa madeni yao kulingana na sifa zao, akisisitiza kuwa juhudi hizo zinaonyesha dhamira ya dhati ya Serikali kuboresha maslahi ya walimu nchini.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.