• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

DC Mbinga atoa rai kwa wenye ulemavu kuchangamkia fursa ya mikopo

Imewekwa kuanzia tarehe: April 17th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Mhe. Cosmas Nshenye amewataka watu wenye ulemavu kuchangamkia fursa ya mikopo inayotolewa na serikali kwa kuhakikisha wanarejesha fedha wanazokopa kwa wakati na kuiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kusimamia suala hilo kikamilifu ili fedha hizo ziweze kunufaisha watu wengine.

Mhe. Nshenye amesema hayo wakati wa kikao cha kutathmini changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu Wilayani Mbinga kilichofanyika leo Aprili 16 katika Ukumbi wa Safina uliopo Kigonsera, huku pia akiwataka watu hao kujiamini na kukubaliana na hali ya ulemavu waliyonayo kwa kusema watu wenye ulemavu wana haki zote na wajibu kama watu wengine.

Akizungumza kwenye kikao hicho, Mhe. Mkuu wa Wilaya amesema watu wenye ulemavu wanapaswa kujiona wenye bahati kwani serikali imewajali kwa kuwatengea asilimia maalumu ya fedha za mikopo licha ya watu hao kuwa na sifa nyingine za ziada za kupatiwa mikopo hiyo kupitia makundi ya vijana na wanawake.

Sambamba na hilo, pia Mhe. Nshenye ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kuhakikisha suala la urejeshwaji wa fedha za mikopo linasimamiwa kikamilifu na kwa mujibu wa sheria na kuwaasa watu wenye ulemavu kuacha kulalamika na kufuta mawazo ya kujinyanyapaa huku akiwataka watu hao kuwa na fikra za kijasiriamali na kujipanga kurejesha fedha za mikopo kama inavyofanywa na wajasiriamali wengine wanaonufaika na mikopo ya 10% ya fedha za mapato ya ndani zinazotengwa na kutolewa na Halmashauri hiyo.

“Watu wa Halmashauri ukifika muda sheria hizi zitumike bila ubaguzi, hawa wote ni wajasiriamali na fedha hizi ni za watu wote..,hatuwezi kuwa na na vikundi visivyorejesha mikopo yao”. Ameongeza Mkuu huyo wa Wilaya.

Bw. Paschal Ndunguru, ambaye ni Afisa Maendeleo ya Jamii, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga amesema Halmashauri hiyo imekua ikitoaji mikopo ya wajasiriamali kwa vikundi vya watu wenye ulemavu kama sehemu ya jitihada zake za kuwezesha watu wenye ulemavu lakini vikundi hivyo vimekuwa na mwitikio hafifu wa kurejesha fedha hizo jambo linalopelekea kushindwa kuwezesha vikundi vingine vingi zaidi na kwa wakati.

Bw. Paschal amefafanua kuwa kwa miaka mitatu mfululizo kuanzia 2018/2019 hadi mwaka huu 2020/2021 Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga imewezesha fedha jumla ya shilingi Milioni 98 kwa vikundi vya watu wenye ulemavu lakini fedha ambazo zimerejeshwa hadi sasa ni Milioni 30.6 pekee.

Awali wakizungumza mbele ya Mkuu wa Wilaya, viongozi wa Chama cha Watu Wenye Ulemavu (CHAWATA) na Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemamavu (SHIVYAWATA) Wilayani Mbinga wameshukuru kwa uwezeshwaji wa fedha ambao umekua ukifanywa na uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga lakini pia wanaomba serikali kuendelea kuwajengea uwezo kwa kuwapa elimu ya ujasiriamali.

Pia viongozi hao wameiomba serikali kuona uwezekano wa kuweka ruzuku kwenye nyenzo na vifaa saidizi kwa watu wenye ulemavu ikiwa ni pamoja na kuweka watoa huduma ambao ni wakalimani wa lugha za alama kwenye maeneo ya kutolea huduma kama hospitali, mahakama, na vituo vya polisi.

Imeandikwa na:

Salum Said

Afisa Habari Halmashauri ya Mbinga

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.