• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

DC NYASA aweka jiwe la msingi ujenzi wa sekondari mpya

Imewekwa kuanzia tarehe: April 10th, 2021

Mkuu wa wa Wilaya ya Nyasa Mh. Isabela Chilumba, amewataka  wananchi Wilayani hapa,kushirikiana na  kutatua Changamoto zinazowakabili hasa za Ujenzi wa Miundombinu ya Shule bila kuisubiri Serikali.

Ameyasema hayo jana wakati akiweka Jiwe la Msingi, katika Shule mpya ya Sekondari Luhangarasi , na Kukabidhi Cheti cha Usajili kwa Uongozi wa Kata Ya Luhangarasi Tarafa ya Mpepo, Wilayani Nyasa.

Akizungumza na wananchi wa Kata hiyo Mkuu huyo, amewapongeza wananchi, kwa kushiriki kikamilifu ujenzi wa Miundombinu  ya Madarasa manne, Jengo la Utawala na matundu nane ya Vyoo yaliyotumia zaidi ya Sh Milioni 60, Zilizochangwa na wananchi ,  kwa Lengo la Kutatua changamoto ya ukosefu wa Shule ya Sekondari, katika Kata hiyo na kuwalazimu wanafunzi kutembea umbali wa km 09 kufuata Sekondari katika Kata jirani  ya Kingerikiti.

Chilumba amefafanua kuwa, wananchi wa Kata ya Luhangarasi ni Mfano wa kuigwa katika Wilaya ya Nyasa, kwa kuwa mara baada ya kuona wana tatizo la ukosefu wa shule ya Sekondari waliamua Kushirikiana na kujenga Shule yao kwa Asilimia mia moja, bila kuisubiri Serikali.

Aidha ametoa wito kwa Wananchi wa Wilaya ya Nyasa Kuiga Mfano huu, wa kujitatulia matatizo yao wenyewe ili kujiletea maendeleo kwa haraka.

Awali akisoma Taarifa ya Shule hiyo Kaimu Afisa Mtendaji Wa Kata hiyo amesema Ujenzi huo ulianza mwaka 2019 kwa vikao halali na vilivyowashirikisha wananchi, wakakubali kutatua changamoto ya watoto wao kutembea Umbali wa km 09 kufuata Shule, hali iliyokuwa ikiwapa usumbufu mkubwa kuweza kufuatilia maendeleo ya shule.

Aidha wananchi hao wameupongeza Uongozi wa Wilaya ya Nyasa, kwa juhudi zao za kuhakikisha shule hiyo inapata namba ya Usajili namba S.5524 Luhangarasi sekondari na kuwapeleka wanafunzi kuanza masomo katika shule hiyo mapema mwaka huu 2021, kwa wanafunzi 188 wa Kidato cha kwanza kudahiliwa, shuleni hapo.

Naye Ofisa Elimu Sekondari  Wilaya ya Nyasa Mwl Rogers Semwalekwa , amewapongeza wananchi hao kwa kutatua changamoto ya ukosefu wa Shule, na ameunga mkono kama Halmashauri kwa kutoa Vifaa vya kufundishia vyenye thamani ya Tsh 1,200,000, pia tayari shule imeingizwa kwenye mfumo wa malipo ya Pranrep kwa ajili ya kupewa Fedha za ruzuku za elimu bila malipo, kutoka Serikalini, na tayari akaumti ya Shule imefunguliwa, na kuendelea kutatua changamoto mbalimbali Shuleni hapo ili kuunga mkono jitihada za wakazi wa Luhangarasi.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa Bw. Jimson Mhagama amewapongeza wananchi hao  na kuwataka kuendeleza juhudi hizo ili kutatua changamoto zingine na kuwaahidi Serikali inaendelea kushughulikia Utatuzi wa Changamoto zingine zinazoikabili shule hiyo.

Imeandikwa na Afisa Habari Wilaya ya Nyasa

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.