• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

DC Tunduru amrejesha shule mwanafunzi aliyeolewa

Imewekwa kuanzia tarehe: July 16th, 2023

MKUU wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma Julius Mtatiro,amevunja ndoa na kufanikiwa kumrudisha shule mwanafunzi (jina linahifadhiwa)aliyekatishwa masomo baada ya kulazimishwa kuolewa na wazazi wake kwa mahali ya Sh.30,000.

Mwanafunzi huyo aliyechaguliwa kuendelea na masomo yake ya kidato cha tano katika shule ya sekondari ya wasichana Masasi,alifunga ndoa ya kimila mapema mwaka huu na kijana anayefahamika kwa jina la Mohamed Salum mkazi wa kijiji cha Muungano mara baada ya kumaliza masomo ya kidato cha nne mwaka jana.

Akizungumza mbele ya Waandishi wa Habari ofisini kwake mjini  Tunduru alisema,kwa sasa mwanafunzi huyo amekabidhiwa katika taasisi moja wilayani humo inayojihusisha na malezi na kufadhili vijana.

Mtatiro alieleza kuwa,serikali ya wilaya inakamilisha taratibu za kumtafutia shule nyingine tofauti na aliyopangiwa  hapo awali ili aweze kuendelea na masomo yake ya kidato cha tano.

Mtatiro alisema,ni kosa kisheria kwa wazazi au walezi kumuozesha mtoto anayepaswa kuendelea  na masomo yake kwa sababu ni kinyume cha sheria na maadili.

Aliongeza kuwa,vitendo na tabia hiyo  vimekuwa chanzo cha kuuwa ndoto za watoto wa kike katika maeneo mengi hapa nchini, na kuwaasa wazazi kuachana na mambo ya kizamani ya kuoza mabinti ambao wana nafasi ya kutoa mchango wao  kwa Taifa.

“wale wote waliohusika katika kumuoza yule mwanafunzi watachukuliwa hatua mara tu taratibu za kisheria zitakapo kamilika,mambo  ya namna hii yanapotokea lazima wanasheria wetu wakae na kuona namna gani ya kuendelea na hatua nyingine,sisi tunasubiri maelekezo nani anashitakiwe na kwa kosa lipi”alisema Mtatiro.

Alisema,serikali itaendelea kuwasimamia na kutoa ulinzi kwa watoto wa kike kama  anavyopigia Rais Samia Suluhu Hassan ya kutaka watoto hao wanakuwa salama na wanaendelea na masomo yao ili waweze kutimiza ndoto za maisha yao.

Amewaonya wazazi wilayani humo,kutojarib kukatisha ndoto za watoto wa kike,badala yake kuhakikisha wanawapa nafasi na kuwasimamia kwa karibu ili wapate elimu bora itakayowasaidia katika maisha yao ya baadaye.
Alisema,elimu ndiyo ufunguo pekee utakaowapa njia wa kike kukabiliana na changamoto na mazingira ya kimaisha yanayokwenda kwa kasi kubwa ndani ya mfumo wa sasa wa Sayansi na Teknolojia na kuwataka wazazi kuwapa nafasi  watoto wa kike ili kuendelea na masomo yao.
Baba mzazi wa mtoto huyo Athuman Ali,amefika ofisini kwa Mkuu wa wilaya na kuomba radhi kwa kumuoza mtoto wake akiwa bado mwanafunzi na kuishukuru serikali kwa hatua iliyochukua ya kumrudisha shule mtoto wake.
“nawaomba wazazi wenzangu ujinga niliofanya mimi  na wao wasifanye,mimi na mke wangu tunajutia kitendo  tulichofanya kumuozesha mtoto wetu aliyechaguliwa kuendelea na masomo yake,pia naiomba serikali itusamehe sana kwa kosa tulilofanya”alisema.

Amewataka wazazi wengine kuacha tabia hiyo badala yake kuwapa nafasi watoto wao kuendelea na masomo ili waweze kutimiza ndoto za maisha yao.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.