Meneja wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) Kampasi ya Songea, Dkt. Bakari Mashaka, amesema wanatarajia kuanza mradi mkubwa wa ujenzi wa chuo kitakachokuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi 10,000 wa kozi mbalimbali katika kata ya shule ya Tanga Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.
Dkt. Bakari Mashaka amebainisha kuwa chuo hicho kinaleta mradi Mkubwa wa bilioni 18.5 za Kitanzania ambazo ni fedha za Serikali kujenga Chuo Kikuu Katika Mtaa wa Pambazuko kata ya Tanga Manispaa ya Songea.
Amesema fedha hizo zimetolewa na serikali chini ya Uongozi wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ambaye amedhamiria kila Mkoa hapa nchini uwe na Chuo Kikuu,hii ni ahadi ambayo aliitoa kwa wananchi na sasa anaitekeleza kwa vitendo kwa wananchi wa Mkoa wa Ruvuma’’,alisema Dkt.Mashaka.
Amesema kwa sasa, IAA Kampasi ya Songea inatoa huduma zake kwenye jengo la TTCL, ghorofa ya pili, mjini Songea, na Kozi zinazotolewa ni diploma ya Usimamizi wa Biashara, Uhasibu na TEHAMA, Fedha na Benki, pamoja na masomo ya ngazi ya uzamili (Masters) katika fani za Biashara, Fedha, TEHAMA, Uongozi, na Usimamizi wa Rasilimali.
Dkt. Mashaka amesema kuwa chuo hicho kinalenga kuhakikisha wanafunzi wanajifunza kwa vitendo, hasa namna ya kuanzisha na kuendesha biashara ambapo ameeleza kuwa wanataka wanafunzi wao wasitegemee ajira pekee, bali wawe na uwezo wa kujiajiri na kuendesha maisha yao.
Kwa upande wake, Afisa Uhusiano wa IAA Kampasi ya Songea, Nuru Meshack, ameelezea changamoto kubwa waliyoibaini katika Wilaya ya Songea ni wazazi wengi kuamini kuwa mtoto aliyepata daraja la nne hawezi kuendelea na masomo, hivyo amewahimiza wazazi na wanafunzi kuwa ufaulu wa D nne, isipokuwa kwa masomo ya dini, unaruhusu mwanafunzi kujiunga na chuo.
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: 0252602256
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.