• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HALMASHAURI ya Mbinga kufuatilia uchimbaji wa madini ya makaa ya mawe

Imewekwa kuanzia tarehe: May 16th, 2021

Kamati Maalum ya Wataalamu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga imeanza zoezi la kufanya ufuatiliaji wa shughuli zinazofanywa na makampuni ya uchimbaji wa madini ya makaa ya mawe yaliyopo Wilayani Mbinga.

Kamati hiyo ambayo imeundwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga inashughulikia masuala mbalimbali ikiwemo mwenendo mzima wa shughuli za uchimbaji na uchakataji wa makaa ya mawe, uzingatiaji wa masuala ya kimazingira, fidia ya ardhi na migogoro baina ya kampuni hizo na jamii inayozunguka maeneo ya migodi.

Timu hiyo imeanza kutekeleza majukumu yake Jumatano Mei 11 kwa kutembelea bandari kavu zote zilizopo Amani Makolo, Mkeso na Paradiso maeneo ambavyo pia ni vituo maalum vya uchakataji na mauzo ya makaa ya mawe vinavyoendeshwa na Kampuni za Mil Coal Ltd, Tan Coal energy Ltd, na Ruvuma Coal Ltd.

Kwa upande mwingine timu hiyo imetembelea na kukagua shughuli za uchimbaji wa madini ya makaa ya mawe kwenye mgodi unaoendeshwa na Kampuni ya Ruvuma Coal uliopo kijiji cha Paradiso na Sara.

Zoezi la ufuatiliaji wa shughuli za uchimbaji wa makaa ya mawe litaendelea tena Jumatatu Mei 17 kwa Kamati hiyo kutembelea Kijiji cha Sara ambapo watakutana na kuzungumza na wananchi wa vijiji vya Sara na Paradiso pamoja na wawakilishi wa Kampuni ya Ruvuma Coal ajenda kuu ikiwa ni suala la fidia kwa maeneo ya wananchi ambayo yapo ndani ya eneo la leseni mbili za uchimbaji wa makaa ya mawe zinazomilikiwa na Kampuni ya Ruvuma Coal.

Timu hii maalum ya ufuatiliaji wa shughuli za uchimbaji wa makaa ya mawe inaundwa na Mwenyeki wa Kamati, Bw. Paschal Zacharia (Afisa Maendeleo ya Jamii), Bw. Salum Said (Kaimu Afisa Mazingira) ambaye ni Katibu na wajumbe ambao ni Bi. Clementina Komba (Afisa Ardhi), Mponjoli Mwakalonge (Mwanasheria) na Waziri Geho ambaye pia ni Afisa Mtendaji Kata ya Ruanda.

Imeandikwa na Salum Said,

Afisa Habari, Mbinga D.C

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.