• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HALMASHAURI ya Mji Mbinga yatumia milioni 650 kujenga nyumba nane za watumishi

Imewekwa kuanzia tarehe: July 11th, 2020

HALMASHAURI YA MJI MBINGA ILIVYOFANIKIWA KUJENGA NYUMBA NANE ZA WATUMISHI KWA MILIONI 650

HALMASHAURI ya Mji wa Mbinga Mkoani Ruvuma, imetumia shilingi milioni 650 kwa ajili ya kutekeleza mradi wa ujenzi wa nyumba saba za wakuu wa Idara na nyumba moja ya Mkurugenzi

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Grace Quintine  amesema Halmashauri yake katika kipindi cha mwaka 2019/2020 ilipokea kiasi cha sh.milioni 350 kwa ajili ya nyumba saba za wakuu wa Idara na kwamba shughuli za utekelezaji zilianza Machi 26 ambapo hadi sasa mradi umefikia asilimia 75.

“Jumla ya shilingi milioni 284.374 zimetumika hadi sasa kati ya milioni 350,vifaa vyote vya viwandani  kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo vimenunuliwa’’,alisema Quintine.

Amesema mradi ulitarajiwa kukamilika Juni mwaka huu,hata hivyo kutokana na changamoto ya kuchelewa kupokea bati ambazo ziliagizwa moja kwa moja kiwandani ALAF ilisababisha mradi kusimama kwa wiki mbili ambapo sasa mradi unatarajia kukamilika mwishoni mwa Julai mwaka huu.

Amesema miradi yote miwili  inatekelezwa kwa kutumia force account ambapo kuna kamati tatu zinazosimamia mradi huu ikiwemo kamati ya ujenzi,kamati ya manunuzi na kamati ya mapokezi na ukaguzi.

Akizungumzia mradi wa ujenzi wa nyumba ya Mkurugenzi,Quintine  amesema katika kipindi cha mwaka 2019/2020 Halmashauri iliidhinishiwa kutumia milioni 300 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya Mkurugenzi ambayo ujenzi wake umefikia asilimia 65.

Amesema mradi huo pia unatekelezwa kwa force account na kwamba licha ya changamoto zilizochelewa mradi,hadi kufikia mwishoni mwa Julai mwaka huu,mradi wa nyumba ya Mkurugenzi unatarajia kukamilika kwa asilimia 100.

Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma ikiongozwa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Musa Homera ilikagua miradi yote miwili  na kuridhishwa na utekelezaji wake ambao unakwenda kuondoa changamoto ya nyumba za kuishi kwa wakuu wa Idara na Mkurugenzi katika Halmashauri ya Mji Mbinga.

Homera ametoa rai kwa Halmashauri nyingine za Mkoa wa Ruvuma kuiga mfano wa Halmashauri hiyo ambapo sasa serikali itaondokana na kuwalipia wakuu wa Idara posho ya nyumba na fedha hizo kutumika katika shughuli nyingine za kuwaletea maendeleo wananchi wa Mbinga.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari wa Mkoa wa Ruvuma

Julai 10,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.