• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

CHIFU aliyezikwa akiwa ameketi Mbinga miaka 140 iliyopita

Imewekwa kuanzia tarehe: July 4th, 2025

Katika kijiji cha Mbuji, wilayani Mbinga mkoani Ruvuma, ndipo unakutana na historia ya kipekee kwenye mawe ya kaburi la mviringo. Hii ni simulizi ya damu, ushindi, usaliti na heshima ya mwisho kwa shujaa wa kale wa Wamatengo.

KABURI LINALOZUNGUMZA

Katika kijiji cha Mbuji, yapo mawe yaliyopangwa kwa ustadi wa heshima. Hapo ndipo alipozikwa Chifu Kayuni Kapitangana Ndunguru Makita  Mtawala wa kwanza wa Wamatengo na Amiri Jeshi Mkuu wa mapambano ya miaka ya moto dhidi ya Waarabu na Wangoni.

Chifu Makita si tu alikuwa kiongozi, bali alikuwa ngao ya taifa lake. Aliongoza mapambano makali kutoka mwaka 1824 hadi 1885, alipouawa kikatili kwa usaliti. Mwili wake ulizikwa ukiwa umekalishwa ishara ya heshima kwa mashujaa wa kale waliotangulia.

USHUJAA WA CHIFU MAKITA

Makita hakuwa tu mpiganaji jasiri bali pia mfanyabiashara mashuhuri aliyewavutia wengi kwa uwezo wa kipekee wa kuongoza.

 Kwa mujibu wa Mheshimiwa Ngwatura Ndunguru aliyewahi kuwa Mbunge wa Mbinga na Afisa Wanyamapori,Makita alijijengea jina kwa hekima na ujasiri wake wa kupambana na hatari kubwa.

“Alianza kama shujaa, si chifu. Lakini mashujaa waliomzunguka walimtambua na kumpa mamlaka kwa sababu ya uwezo wake wa kuongoza na kushinda vita,” anasema Ndunguru.

 

USALITI ULIOGEUKA URITHI

Katika kile kinachoaminika kuwa hila ya Waarabu waliokuwa washirika wa kibiashara, Makita aliuawa kwa hadaa na kukatwa kichwa. Kichwa hicho kilikimbizwa kama ishara ya kushusha hadhi yake lakini haikufanikiwa.

Simulizi ya shujaa wa kike, Kingengi, ambaye kwa ujanja na imani za kiroho aliweza kukirudisha kichwa hicho kijijini, ni mfano halisi wa uzalendo na mapenzi kwa taifa. Aliwarubuni maadui kwa michezo ya jadi, akafanikiwa kuiba kichwa cha chifu wake waliokipora.

Usiku huohuo, wazee walikusanyika. Walikifunga kichwa kwenye kiwiliwili cha shujaa wao na kumzika kwa heshima ya kipekee, akiwa amekalishwa kwenye kaburi la mviringo. Vijana sita mashujaa, waliamua kuzikwa hai pamoja naye,wakiamini kuwa mtu mkubwa hawezi kwenda "ng’ambo ya pili" peke yake.

URITHI WA KISHUJAA ULIOFICHWA

Leo, zaidi ya miaka 140 baadaye, kaburi la Makita limesimama kijijini Mbuji kama ishara ya utambulisho wa Wamatengo. Mawe yaliyolizunguka yalipangwa upya mwaka 2004 na familia yake, kwa kushirikiana na viongozi wa kijiji wakati Ngwatura Ndunguru alipokuwa mbunge.

“Hadithi za mashujaa wetu bado hazijaandikwa vya kutosha. Serikali inapaswa kushirikiana na baraza la mila la Wamatengo kuhakikisha historia kama hii haipotei. Ni urithi wenye thamani kubwa ya kitaifa na kimataifa,” anasisitiza Ndunguru.

NI MUDA WA KUIFUKUA HISTORIA

Hadithi ya Chifu Makita si tu ya huzuni. Ni mwito wa kizalendo,sauti ya historia inayohitaji kusimuliwa upya. Mbinga inabeba kaburi lenye simulizi ya kiongozi aliyezikwa akiwa ameketi, akilindwa na mashujaa sita waliompenda mpaka mwisho.

Ni wakati wa Serikali, wanahistoria, na vijana wa sasa kuifufua simulizi hii na kuiweka katika vitabu vya historia, majukwaa ya kitaifa na maonesho ya utalii wa kiutamaduni.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • CHIFU aliyezikwa akiwa ameketi Mbinga miaka 140 iliyopita

    July 04, 2025
  • NGORO ufumbuzi wa kilimo endelevu

    July 04, 2025
  • NMB wamtembelea RC Ruvuma

    July 02, 2025
  • KITUO cha mabasi cha Lundusi Peramiho chazinduliwa rasmi

    July 02, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.