• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC RUVUMA akabidhi mkataba wa ujenzi masoko ya Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: July 6th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, amemkabidhi mkandarasi kutoka kampuni ya China National Aero Technology International Engineering Corporation (AVIC) mkataba wa ujenzi wa masoko ya kisasa ya Manzense A na B yatakayojengwa katika Kata ya Misufini, pamoja na kiwanda cha kuchakata mazao ya nafaka katika Kata ya Lilambo, Halmashauri ya Manispaa ya Songea.

Hafla ya makabidhiano ya mkataba huo imefanyika katika Kata ya Misufini, ambapo Kanali Ahmed amemuagiza mkandarasi kuhakikisha kuwa ujenzi huo unakamilika ndani ya muda uliopangwa, kwa kuwa wananchi wameusubiri kwa muda mrefu na wana matarajio makubwa.

Kwa kuzingatia thamani ya miundombinu hiyo, amewataka wananchi kushiriki kikamilifu katika kulinda rasilimali zote zilizoandaliwa kwa ajili ya ujenzi huo, na kuhakikisha kuwa masoko hayo yanatunzwa ipasavyo mara baada ya kukamilika.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea, Wakili Bashir Muhoja, ameeleza kuwa jumla ya shilingi bilioni 22.9 zitatumika katika ujenzi wa masoko hayo pamoja na kiwanda cha kuchakata mazao ya nafaka ambapo  Kampuni ya China National Aero Technology International Engineering Corporation (AVIC) ndiyo iliyopatiwa zabuni ya kutekeleza mradi huo.

Amebainisha kuwa mradi huo unatarajiwa kuanza rasmi tarehe 15 Julai 2025 na kukamilika ifikapo 15 Julai 2026 na utekelezaji wake unatarajiwa kuleta matokeo chanya kwa kuboresha mazingira ya biashara, kuongeza thamani ya mazao ya wakulima, na kutoa fursa za ajira kwa wananchi wa Songea na maeneo ya jirani.

Kwa upande wa Sekretarieti ya Mkoa, Jumanne Mwankhoo, akimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma, ameeleza kuwa kwa kuzingatia maelekezo ya Waziri wa TAMISEMI, mradi huo utasimamiwa kwa karibu ili kuhakikisha unakamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyotakiwa.

Mkandarasi kutoka kampuni ya AVIC, Bw. Kevin Long, ameahidi kukamilisha mradi huo kwa wakati na kushirikisha wananchi katika ajira mbalimbali zitakazopatikana wakati wa ujenzi.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KISIWA cha Lundo Almas iliyojificha ziwa Nyasa

    July 07, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 216 kwa ajili ya chanjo ya mifugo

    July 06, 2025
  • RC RUVUMA akabidhi mkataba wa ujenzi masoko ya Songea

    July 06, 2025
  • CHIFU aliyezikwa akiwa ameketi Mbinga miaka 140 iliyopita

    July 04, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.