• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HALMASHAURI ya Namtumbo yapata hati safi

Imewekwa kuanzia tarehe: June 13th, 2022


HALMASHAURI ya Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma imepata hati safi  katika matokeo ya ukaguzi ambao ulifanywa kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30,2021.

Akizungumza katika kikao maalum cha Baraza la Madiwani cha kujadili taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG katika Halmashauri ya Namtumbo,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amewapongeza watumishi na Baraza la madiwani kwa kusahihisha makosa walioyafanya mwaka 2019/2020 ambapo Halmashauri hiyo ilipata hati yenye mashaka.

RC Ibuge amesema hati yenye mashaka katika kipindi hicho ilileta doa kwenye rekodi za kupata hati safi ambapo hivi sasa Halmashauri hiyo imerejea kwenye mstari wa kupata hati safi.

“Napenda sasa nitoe maelekezo kama sehemu ya dira katika kujihakikishia kuwa Namtumbo inaendelea kupata hati safi kwa kuhakikisha hoja zote zilizosalia zifungwe,zuieni kujirudia hoja,wakuu wa Idara washiriki ipasavyo kuandaa majibu ya hoja na utekelezaji wa mapendekezo ya CAG’’,alisisitiza Ibuge.

Mkuu wa Mkoa pia ameagiza Halmashauri kuchukua mapema hatua za kinidhamu kwa watumishi wanaozalisha hoja ili isionekane ni jambo la kawaida  na kwamba upotevu wa mapato katika Halmashauri na vyanzo vya upotevu vidhibitiwe na hatua zichukuliwe kwa wahusika.

RC Ibuge pia ameagiza kuwepo umakini mkubwa katika utekelezaji wa sheria,kanuni na taratibu za manunuzi na kwamba Halmashauri iendelee kulipa madeni mbalilmbali ya wazabuni kwa wakati ili iweze kujiendesha kwa tija.

Mkuu wa Mkoa pia ameipongeza Halmashauri ya Namtumbo kwa kuchangia kwa asilimia 87.5 mfuko wa wanawake,vijana na watu wenye ulemavu ambapo wameweza kuchangia shilingi milioni 83.

Hata hivyo amesema Halmashauri ya Namtumbo katika mwaka wa fedha 2020/2021 imeweza kukusanya mapato ya ndani kwa asilimia 82.62 ya lengo la kukusanya Zaidi ya shilingi bilioni 1.77 hivyo kufanikiwa kukusanya Zaidi ya shilingi bilioni 1.46.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kuendelea kuwasimamisha kazi watumishi ambao ni Afisa Manunuzi Samson Manjale na Afisa Maendeleo ya Jamii Pelesta Mugusha ili kupisha uchunguzi unaoendelea kufanywa na Tume maalum.

Brigedia Jenerali Ibuge amemuagiza Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma kufanya uchunguzi mara moja kuhusiana na tuhuma zinazowakabili watumishi hao   ambapo amemtaka Mganga Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo kutoa ushirikiano katika uchunguzi wa TAKUKURU.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ameanza vikao maalum vya Baraza la madiwani katika Halmashauri zote nane ili kujadili taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za serikali.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Juni 13,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.