• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HALMASHAURI ya Nyasa yapokea milioni 226 kujenga OPD Kituo cha Afya Kingeriti na vyoo

Imewekwa kuanzia tarehe: July 6th, 2020

SERIKALI imetoa zaidi ya shilingi milioni 226 katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma kutekeleza ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje OPD  na matundu ya vyoo 17 katika shule ya msingi Ukuli Kata ya Kingerikiti.

Akitoa taarifa ya miradi hiyo kwa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma wakati wa ziara ya ukaguzi wa utekelezaji wa Ilani ya CCM,Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa Jimson Mhagama amesema serikali imetoa kiasi cha sh.milioni 200 kujenga OPD  na matundu sita ya vyoo katika kituo cha Afya Kingerikiti.

Mhagama amesema mradi huo ulianza kutekelezwa Aprili 24 mwaka huu na unatarajia kukamilika Agosti 30 mwaka huu ambapo mradi upo katika hatua ya jamvi ukiwa na asilimia 25 na hatua ya lenta ni  asilimia 47 na kwamba mradi unatekelezwa kwa force akaunti.

“Eneo la mradi lina ukubwa wa  hekari 18,hadi sasa mradi umetoa ajira za muda kwa watu 30,mradi unatekelezwa kwa kushirikiana na wananchi wa kata ya Kingerikiti kutoka vijiji vinne vya Kingerikiti,Ukuli,Lumecha na Mawasiliano.

Akizungumzia mradi wa matundu  17 ya vyoo katika shule ya msingi Ukuli,Mkurugenzi huyo amesema serikali imetoa zaidi ya shilingi milioni 26 kupitia fedha za  udhamini  kutoka SWASH kwa ajili ya utekelezaji wa ujenzi wa mradi huo.

Amesema utekelezaji wa mradi huo ni kwa kutumia force akaunti na kwamba mradi umeanza Juni 3 mwaka huu na  ulitarajiwa kukamilika Juni 30 mwaka huu.

Katibu wa CCM Mkoa wa Ruvuma Nuru Ngeleja amewapongeza wananchi wa kijiji cha Ukulu kwa kufanikisha ujenzi wa miundombinu ya vyoo ambavyo amesema vitawawezesha wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo kuwa na mazingira rafiki ya kusomea na kulinda afya zao.

Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Ruvuma Kuruthumu Mhagama ameipongeza serikali kwa kuamua kujenga kituo cha Afya Kingerikiti ambacho amesema kitakuwa ukombozi wa  wananchi hao ambao walikuwa wanasafiri umbali mrefu kufuata huduma za afya.

Naye Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Musa Homera  amewapongeza watendaji wa Halmashauri ya Nyasa  kwa kusimamia vema miradi ya maendeleo ambayo mingi imekamilika na imeanza kuwanufaisha wananchi.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Juni 5,2020

Nyasa

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.