• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HALMASHAURI ya Songea yajenga shule mpya yenye mahitaji maalum

Imewekwa kuanzia tarehe: October 31st, 2022

HALMASHAURI  ya wilaya ya Songea mkoani Ruvuma,imepokea kiasi cha Sh.milioni 380 kutoka Serikali kuu kwa ajili ya kujenga vyumba 19 vya madarasa kwenye shule shikizi zilizojengwa kwenye maeneo yenye mazingira magumu ya kupata elimu kwa wanafunzi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Neema Maghembe alisema,fedha hizo zimetumika kujenga jumla ya shule mpya tano za msingi ikiwamo shule ya Lihuhu  ili kuwanusuru watoto wenye umri wa kuanza shule kukosa haki ya kupata elimu.

Maghembe alisema,awali wanafunzi wanaotoka katika kijiji  cha Lihuhu walilazimika kutembea umbali wa km 7 kwenda kijiji cha Lilahi kufuata shule, hivyo kusababisha baadhi yao kukatisha masomo.

Alisema,katika kijiji hicho  ambacho mwanzo kilikuwa kama kitongoji cha kijiji mama cha Lilahi,serikali imejenga jumla ya madarasa matatu kwa gharama ya Sh.milioni 60 ikiwa ni mkakati wake wa  kuimarisha na kuboresha miundombinu ya elimu.

Alisema,baada ya kukamilika kwa ujenzi wa vyumba hivyo,sasa wanafunzi wamekuwa na mazingira mazuri ya kujisomea na walimu kuwa na muda mzuri ya kufundisha ikilinganishwa na awali ambapo kulikuwa na madarasa ya miti yaliyojengwa na wananchi.

Maghembe alitaja shule zilizojengwa kupitia fedha hizo ni Jenista Mhagama, ambapo serikali imejenga vyumba vitatu kwa gharama ya Sh.milioni 60 na shule ya msingi Lunyele madarasa matatu kwa Sh.milioni 60.

Shule nyingine zilizonufaika na fedha hizo ni Mhimbasi iliyopata  madarasa matano kwa gharama ya Sh.milioni 100 na kata ya Kizuka ambapo imejengwa shule mpya yenye madarasa Matano kwa gharama ya Sh.milioni 100.

Alisema,serikali inaendelea kufanya juhudi kubwa kuhakikisha kila mtoto mwenye umri wa kuanza elimu ya awali,msingi na sekondari anapata elimu na kuwaomba wazazi,walezi na jamii kwa ujumla kushiriki na kujitolea nguvu zao kujenga na kuboresha miundombinu ya elimu.

Baadhi ya walimu wa shule hizo, wameipongeza Serikali kwa jitihada zake za kujenga na kuboresha miundombinu ya elimu katika maeneo mbalimbali.

Mwalimu mkuu wa shule ya Lihuhu Simon Pascal alisema kuwa, madarasa hayo mapya yamehamasisha sana wanafunzi kuhudhuria masomo na kukomesha tatizo la utoro  na kurudisha morali ya kufundisha kwa walimu.

Mwalimu Pascal alisema,baada ya kujengwa madarasa mpya hata idadi ya watoto wanaoanza darasa la kwanza imeongezeka kutoka 20 mwaka wa masomo 2020/2021 hadi 45 kwa mwaka wa masomo 2021/2022.
Mwalimu wa shule ya msingi Lunyele kata ya Muhukuru Silvesta Ngumba,ameiomba serikali kupitia Halmashauri ya wilaya kuwasaidia walimu wanaofanya kazi kwenye maeneo yenye mazingira magumu kwa kutoa motisha na kuboresha mazingira yao.

Alisema,licha ya serikali kujenga vyumba vipya vya madarasa kwa ajili ya kuboresha mazingira ya kujifunza na kufundishia,hata hivyo kwa upande wa walimu bado wanakabiliwa na mazingira magumu.
Alisema,changamoto kubwa hasa ni makazi kwani katika shule hiyo kuna walimu watano ambao wanaishi kwenye nyumba moja ambayo haina hadhi ya kuishi mtumishi wa umma.

Aidha alisema, hata wanapohitaji kufika makao makuu ya Halmashauri ya wilaya au Songea mjini, wanalazimika kutumia zaidi ya shilingi 50,000 kama nauli,hivyo ameiomba serikali kuwaangalia kwa jicho la huruma watumishi waliokubali kufanya kazi kwenye mazingira hayo.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.