• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HALMASHAURI ya Wilaya ya Songea yagawa pembejeo bure za zao la ufuta kwa wakulima

Imewekwa kuanzia tarehe: December 8th, 2020


Halmashauri ya wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma imegawa mbegu ya ufuta bure kwa wakulima wa zao la ufuta katika Kata ambazo zinazalisha zao hilo kwa wingi kwa msimu wa kilimo wa mwaka 2020 /2021.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuri hiyo Bw Simon Bulenganija amesema ametumia kiasi cha sh. milioni 10 kwa ajili ya kununua mbegu hiyo kwa lengo la kuwasaidia wakulima ili waweze kuongeza uzalishaji kutoka gunia tatu hadi tano kwa ekari moja,tofauti na awali wakulima walikuwa wakizalisha gunia moja hadi tatu kwa ekari moja kwakutuia mbegu ya kienyeji.

Ametaja idadi ya kilo zilizonunuliwa na kusambazwa kwa wakulima kuwa ni kilo 1000 na aina ya mbegu ni Lindi 02 zilizonunuliwa kutoka Kituo cha Utafiti wa Mazao cha Naliendele kilichopo Mkoani Mtwara.

Amezitaja kata na idadi ya kilo zilizosambazwa kuwa ni kata Muhukuru Barabarani na Lilahi ambao wamepata kilo 225,Kata ya Matimira kilo 180,Kilagano kilo 180,Kizuka 180,Ndongosi kilo 90 na Magagura kilo 90.

Bulenganija ameyataja malengo ya kusambambaza mbegu hiyo ni kuwapunguzia wakulima gharama ya kununua mbegu ya ufuta ambayo huuzwa shilingi 10,000 kwa kilo moja pia kuongeza uzalishaji na Serikali iweze kupata mapato kupitia ushuru unaotolewa na wakulima mara baada ya kuuza kupitia vyama vyao vya ushirika.

Kwa upande wake Afisa Kilimo Mazao wa Halmashauri hiyo Norbert Rugonza amewashauri wakulima wa zao la ufuta wasitegemee matokeo chanya kwenye kilimo bila kusimamia vizuri na kufuatilia wakati wa uzalishaji.

Amesema wakulima ambao wamebahatika kupata mbegu hizo wanatakiwa kuzitumia kama shamba darasa kwakuzalisha kwa wingi na kusambaza kwa wakulima wengine kwenye msimu wa kilimo wa mwaka 2021 /2022.

Amesema mbegu ya aina ya lindi 02 ni mbegu bora na nzuri kwa kilimo cha ufuta kwa sababu ni mbegu ambayo inastahimili magonjwa hivyo ni vema wakulima wakaachana na dhana potofu ya kwamba mbegu za kisasa zina matatizo ya kushambuliwa na magojwa na wadudu jambo ambalo halina ukweli.

Kwa upande wake Afisa Ushirika wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Shekiel Masawe amesema katika msimu wa mwaka 2018/2019 ilifanikiwa kuzalisha zao la ufuta kilo milioni 1,316,227 na katika msimu wa kilimo wa mwaka 2019/2020 ilizalisha zao la ufuta kilo milioni 2,378,172 na kufanikiwa kuingiza mapato ya Zaidi ya shilingi milioni 400.

Imeandaliwa na

Jacquelen clavery

Songea DC

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.