• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HATUWEZI kuliingiza Taifa kwenye njaa-RC Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: November 26th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amesema hayupo tayari kuliingiza Taifa kwenye njaa kwa kuendekeza wafugaji na kwamba ni marufuku wafugaji kuingia kwenye maeneo ya wakulima.

Akizungumza kwa nyakati tofauti na watumishi wa Halmashauri za Madaba na Songea ,Kanali Thomas amesisitiza kuwa Mkoa wa Ruvuma sio Mkoa wa wafugaji bali ni Mkoa wa kilimo ambao unaongoza kitaifa kwa kuzalisha mazao ya chakula .

“Ruvuma sio Mkoa wa wafugaji ni Mkoa wa wakulima,hatuwezi kuliingiza taifa kwenye njaa kwa kuendekeza wafugaji “,alisisitiza RC Thomas.

Amesema operesheni ya kuwaondoa Mifugo yote iliyopo katika maeneo ya wakulima itafanyika katika Mkoa mzima kuanzia Desemba 10 mwaka huu.

Ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya Madaba kuwatafuta wafugaji wenye makundi makubwa ya ng,ombe waliopewa dhamana  baada ya mifugo yao kukamatwa ikila mazao ya wakulima ili warudi kulipa  faini.

Hata hivyo amewapongeza wakulima wa Madaba kutumia busara kubwa kwa sababu wangechukua sheria mkononi yangetokea maafa makubwa kati ya wakulima na wafugaji.

Amesisitiza kuwa wafugaji wote wasiokuwa na kibali waondolewe na kwamba hayupo tayari kuona kundi fulani linakandamiza makundi mengine.

Amesema uchunguzi umebaini kuwa hivi sasa wafugaji hawapandishi Mifugo kwenye magari badala yake wanashushia ng’ombe Wilaya Njombe na kuingia nao kwa miguu mkoani Ruvuma hivyo amemwagiza Kamanda wa Polisi Mkoani Ruvuma kuwadhibiti wafugaji hao .

Ameagiza kuchukuliwa hatua za kisheria kwa mifugo yote inayokamatwa na kwamba watoe taarifa kwake endapo kuna kiongozi yeyote aliyopo chini yake ndani ya Mkoa anakwamisha maagizo yake.

“Hatuwezi kuwa na viongozi wababaishaji ndani ya Mkoa ambao wanadhulumu haki za wananchi ,nilishasema sitaki wafugaji kwenye maeneo ya wakulima “,alisisitiza.

Kwa upande Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mheshimiwa Menasi Komba amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuwadhibiti wafugaji katika maeneo ya wakulima.

Amesema tayari wamefanikiwa kuondoa mifugo zaidi ya 5000 katika eneo la Kikunja Kata ya Matimira na kwamba kwa kushirikiana na jeshi la polisi wanaendelea kuondoa mifugo hiyo katika maeneo mengine ya wakulima.

Hata hivyo amesema mifugo kwa kiwango kikubwa imedhibitiwa katika Halmashauri hiyo hivyo kupunguza kero kubwa ya uharibifu wa mazao ya wakulima.

Mkoa wa Ruvuma ni kapu la Taifa la chakula nchini ambapo kwa miaka minne mfululizo umeongoza kitaifa katika uzalishaji wa mazao ya chakula.

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma 

Novemba 26,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.