• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HIFADHI ya Taifa ta Nyerere,mlango mpya wa utalii unaofungua uchumi wa Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: April 23rd, 2025

Na Albano Midelo

Katika bonde la kijani lililojaa mandhari ya kuvutia kusini mwa Tanzania, wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma sasa inang’aa kama nyota mpya ya utalii.

Kupitia uwekezaji wa Shilingi bilioni 2.1 kutoka Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, lango la kisasa kuingia Hifadhi ya Taifa ya Nyerere limejengwa eneo la Likuyuseka Maganga na sasa, ndio mlango rasmi wa watalii kuingia hifadhi hiyo kupitia Nyanda za Juu Kusini.

 Akizungumza kwa furaha, Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo, Mheshimiwa Ngollo Malenya, anasema ujenzi wa lango hilo umekamilika na sasa wilaya yake ipo tayari kuwakaribisha wageni kutoka kila pembe ya ukanda wa kusini,ikiwemo mikoa ya Lindi, Mtwara, Njombe, Iringa, Mbeya hadi Ruvuma, na hata nchi jirani kama Msumbiji na Malawi.

“Lango hili ni fursa ya kipekee kwa Namtumbo na Mkoa wa Ruvuma. Linakuza uchumi wetu kwa haraka na linafungua njia ya uwekezaji mkubwa kwenye sekta ya utalii,” anasisitiza Malenya huku akitoa rai kwa wawekezaji wa ndani na nje kuwekeza kwenye ujenzi wa hoteli, huduma za utalii na miundombinu mingine muhimu.

Mlango Mpya, Fursa Mpya

Lango la Namtumbo ni mojawapo ya njia muhimu za kuingia Hifadhi ya Taifa ya Nyerere, mojawapo ya hifadhi kubwa zaidi Afrika inayochukua zaidi ya kilomita za mraba 30,000. Hifadhi hii ilianzishwa rasmi mwaka 2019, ikiwa sehemu ya urithi wa zamani wa Selous Game Reserve.

Kupitia lango hili, wageni kutoka mikoa ya kusini sasa wanaweza kufurahia urahisi wa kuingia hifadhi hiyo bila kupitia njia za mbali.

Wageni kutoka Songea, Tunduru na maeneo ya mpakani mwa Msumbiji wanaweza sasa kuingia moja kwa moja kwenye mbuga hiyo tajiri kwa wanyamapori na mandhari ya kuvutia.

Vivutio Vilivyo Karibu na Lango

Eneo hili linajivunia kuwa na wanyamapori wakubwa kama tembo, simba, chui, nyati, na pundamilia wanaoonekana mara kwa mara katika maeneo ya karibu na lango.

Kivutio kingine ni bwawa la Kaunde, linalofahamika kama bwawa la viboko.Ni bwawa la pekee, lililoko juu ya mlima, na lenye sifa ya kushangaza, maji yake hayakauki mwaka mzima, lakini chanzo chake hakijulikani.

Likiwa limezungukwa na milima na msitu mnene wa hifadhi, bwawa hili limebaki kuwa eneo la asili lisiloguswa, kivutio kwa watalii wa ndani na wa kimataifa wanaotafuta uzuri wa Tanzania.

Isitoshe, Namtumbo inaongeza thamani ya utalii kupitia vivutio vya kiutamaduni. Watalii wanaweza kutembelea vijiji vya Wandendeule na Wangoni na kujifunza historia, mila na utamaduni wa watu wa Ruvuma.

Matokeo kwa Jamii

Kwa jamii ya Namtumbo, faida tayari zimeanza kuonekana. Vijana wameanza kupata ajira kama waongoza watalii, madereva, wapishi na wahudumu wa hoteli. Wananchi pia wanashiriki kwenye miradi ya ujirani mwema inayoratibiwa na TANAPA,TAWA na TFS.

Kwa uwepo wa lango la kisasa la Namtumbo, si tu kwamba Ruvuma imejiunga rasmi na ramani ya utalii wa kimataifa, bali pia imepiga hatua kubwa katika kujenga uchumi shirikishi unaowagusa watu wa kawaida.

Karibu Namtumbo,mlango wa kusini unaofungua milango ya fursa  za utalii na uwekezaji zisizo na kikomo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.