• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HOMA ya nguruwe inavyoleta umaskini kwa wafugaji Nyanda za Juu kusini

Imewekwa kuanzia tarehe: August 13th, 2020

Daktari wa mifugo Mkuu Kanda ya Nyanda za Juu Kusini  Dr. Solomon Nong’ona akizungumzia ugonjwa wa homa ya nguruwe katika Kanda hiyo,  anasema Idadi ya nguruwe Tanzania ni karibu milioni 2.14  kati ya hao asilimia 90 wanafugwa na wakulima wadogo.

Dr.Nong’ona anasema wakulima hukosa njia sahihi za kuzuia magonjwa, elimu ya ufugaji na mipango bora ya kuzalisha nguruwe hao  na kwamba ufugaji wa nguruwe katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini una vikwazo vingi na moja ya hivyo ni uwepo Homa ya nguruwe (ASF)

Abainisha zaidi kuwa homa ya nguruwe ni ugonjwa ulioanzia kwa mara ya kwanza katika  Halmashauri ya Kyela katika mkoa wa Mbeya,Kutoka Novemba 2010 hadi sasa mwaka 2020 ugonjwa huo umeathiri karibu kila halmashauri  zilizopo katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.

“Kuanzia Novemba 2019 hadi Machi 2020 mkoa wa Njombe  ndiyo uliokuwa na matukio mengi kwenye Halmashauri za Makambako na Njombe  ya homa ya nguruwe,Ugonjwa umeenea pia katika Mkoa wa Iringa kwenye Halmashauri za Kilolo, Mafinga na Mufindi’’,anasema Dr.Nong’ona.

Hata hivyo Daktari huyo wa Mifugo  anasema,Februari 2011 Homa ya nguruwe imeendelea kutawanyika  katika Halmashauri ya Nyasa kwenye ukanda wa Ziwa Nyasa mpaka katika Mkoa wa Ruvuma kwenye  Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa,Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga,Halmashauri ya Wilaya ya Songea na  Halmashauri ya Manispaa ya Songea.

Anabainisha zaidi kuwa Machi 2011,ugonjwa wa homa ya nguruwe ulikuwa tayari umefika katika Halmashauri za  wilaya za Chunya, Mbarali na Rungwe katika Mkoa wa Mbeya na  Halmashauri ya Wilaya ya  Ileje kwenye Mkoa wa Songwe

Anasema asilimia 60 ya nguruwe waliopo nchini Tanzania wanatoka Nyanda za Juu Kusini katika  mikoa ya  Mbeya, Iringa, Ruvuma, Songwe na Njombe

“Mradi wa nguruwe unaweza kuzalisha faida mpaka shilingi 252,165,100.00 (US$109,637.40) kwa mwaka katika nchi ,Wakati huo huo ugonjwa huu unaweza kusababisha hasara ya mpaka shilingi 2,094,922,800.00 (US$910,836.70)  kwa mwaka katika nchi kwa hiyo mradi wa kufuga nguruwe ni benki inayotembea’’,anasisitiza Dr.Nong’ona.

Anasema mikoa ya Nyanda za Juu kusini ina Halmashauri 31 na kwamba ni  halmashuari 14 tu ndizo hivi sasa  zimeathirika sana na Homa ya nguruwe  ambazo anazitaja kuwa ni Halmashauri ya Mji  Makambako, Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Halmashauri ya Mji Njombe.

Halmashauri nyingine  anazitaja kuwa ni Mbarali, Chunya, Mbozi, Tunduma, Mufindi, Halmashauri ya Mji  Mafinga,Halmashauri ya wilaya ya Mbinga, Halmashauri ya Mji  Mbinga, Halmashauri ya Ludewa,Halmashauri ya Songea na Halmashauri ya Manispaa ya Songea.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Februari 13,2020

Mbeya


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.