• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HOPSITALI ya Kiuma Tunduru yapigwa jeki kifaa cha kisasa kwa wagonjwa

Imewekwa kuanzia tarehe: October 25th, 2022

HOSPITALI ya Kiuma inayomilikiwa na Kanisa la Upendo wa Kristo Masihi wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma,imepokea msaada wa mashine ya X-Ray kwa ajili ya wagonjwa wanaohitaji kufanyiwa uchunguzi magonjwa mbalimbali ikiwamo ya mionzi.

Mashine hiyo imetolewa na shirika la Neno na Tendo(Word&Deed)kutoka nchini Ujerumani ambayo ni ya kwanza kwa ukubwa na ubora,katika Hospitali binafsi na Serikali kwa ukanda wa mikoa ya kusini.

Hayo yamesemwa na Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo Dkt Nzelipa Masaga,wakati akitoa taarifa kwa Mkuu wa wilaya hiyo Julius Mtatiro aliyeambatana na Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini Hassan Kungu na mwakilishi wa shirika la Word&Deed Susanna Diechmann.

Alisema,uhusiano uliopo kati ya Kanisa la Upendo wa Kristo Masihi na Shirika  hilo ndiyo uliowezesha kupatikana kwa mashine hiyo ya kisasa(Digital) ambayo imeanza kuwa msaada mkubwa  watu wanaofika kupata  huduma ya uchunguzi wa magonjwa mbalimbali.

DKT Nzelipa Masaga alisema,mashine hiyo ina uwezo wa kupima na kutambua kwa haraka magonjwa na shida nyingine katika mwilini tofauti na mashine iliyokuwepo zamani(Manual). Alisema, X-ray mpya ni suluhisho kubwa kwa  watu wanaotoka maeneo mbalimbali hasa ikizingatia  kuwa, Halmashauri ya wilaya ya Tunduru imeipa Hospitali hiyo jukumu la kusimamia jumla ya zahanati tisa za vijiji jirani na kituo cha afya kimoja.

Alisema kuwa,kupatikana kwa mashine hiyo ni ukombozi mkubwa kwa wagonjwa wanaofika kupata matibabu na wanaotakiwa kufanyiwa uchunguzi  kwa njia ya mionzi.

Kwa mujibu wa Dkt Masaga,mashine hiyo ina uwezo wa kubaini matatizo ya wagonjwa wengi kwa wakati mmoja itasaidia  kumaliza msongamano wa kusubiri vipimo kwa muda mrefu kwa watu wanaofika katika Hospitali.

Dkt Masaga alisema, kupatikana kwa mashine hiyo kunaashirikia mwanzo wa  katika uboreshaji wa huduma za afya zinazotolewa na Kanisa hilo kwa kushirikiana na wadau shirika la Word&Deed kwani sasa wamefanikiwa hata kupanua huduma za matibabu ikiwamo ya mivunjiko(wanaopata ajali).

Dkt Masaga alifafanua kuwa,siku za nyuma walishindwa kutoa  huduma ya uchunguzi kwa wagonjwa wengi kwa kuwa X-ray iliyokuwepo haikuwa na uwezo wa kutambua matatizo kwa haraka,hivyo baadhi ya wagonjwa walilazimika  kwenda hadi Hospitali ya wilaya Tunduru mjini umbali wa km 67 kufuata huduma  ya X-ray.

Hata hivyo alisema, changamoto kubwa ni upungufu mkubwa wa watumishi kwani mahitaji 105 na waliopo ni 56,na kuiomba serikali kutafuta njia ya kuwasaidia watumishi ambao wataongeza nguvu  ya kuhudumia wananchi wanaofika katika Hospitali ya Kiuma.

Kwa upande wake mwakilishi wa shirika la Word&Deed Susanna Diechmanna amehaidi kuwa, shirika hilo litaendelea kusaidia vifaa mbalimbali kwa Hospitali hiyo ili  iweze kuboresha  na kutoa huduma bor

Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini Hassan Kungu ameripongeza shirika la Word&Deed kwa msaada huo, kwa sababu wananchi wa Jimbo la Tunduru kaskazini na mkoa wa Ruvuma wana uhakika wa kupata huduma ya  mionzi karibu  na  haraka.

Mkuu wa wilaya ya Tunduru Julius Mtatiro,licha ya kuwashukuru wafadhili hao kwa misaada mbalimbali wanayotoa kwa Kanisa la Upendo,amewataka wafanyakazi wa Hospitali hiyo kuhakikisha wanatunza vifaa hivyo ili viweze kudumu kwa muda mrefu.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.