• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HOSPITALI ya Tunduru yaanza msako wa wagonjwa wa kifua kikuu

Imewekwa kuanzia tarehe: June 12th, 2023

SERIKALI kupitia kitengo cha kifua kikuu na ukoma Hospitali ya wilaya Tunduru mkoani Ruvuma,imeanza msako wa  kuwasaka waganga wa tiba asili wanaowarubuni wagonjwa wa kifua kikuu  wasiendelee kutumia dawa za Hospitali ili watumie dawa za asili kwa lengo la kujipatia  fedha.

Mratibu wa kifua kikuu na ukoma wa wilaya ya Tunduru Dkt Mkasange Kihongole alisema,msako huo unakwenda sambamba na kuwatafuta watu wote waliobainika kuwa na maambukizi ya ugonjwa huo walioanzishiwa matibabu lakini wameacha kwenda Hospitali na kutumia dawa  kwa sababu zisizofahamika.

Dkt Kihongole amesema hayo jana,wakati wa zoezi la kuwasaka waganga  hao na wagonjwa wa kifua kikuu katika kijiji cha Nandembo,huku baadhi ya wagonjwa wamekutwa katika kilinge cha mganga wa tiba asili  Mohamed Heja wakipatiwa dawa za asili.

Aidha msako huo unawahusisha wataalam wa kitengo cha kifua kikuu na ukoma wa Hospitali hiyo na watendaji wa vijiji na kata kama njia rahisi ya kuwapata wagonjwa waliokatisha kumeza dawa kama hatua ya kudhibiti kuenea kwa ugonjwa huo.

Alisema,lengo la msako huo ni kuwapata wagonjwa waliobainika kuwa na kifua kikuu na kuanzishiwa matibabu lakini kutokana na sababu zisizojulikana hawafiki Hospitali kupata ushauri na kuendelea kumeza dawa,jambo ambalo ni hatari kwao na jamii inayowazunguka.

Alisema,wilaya ya Tunduru inatajwa kuwa na maambukizi makubwa na wagonjwa wengi wa kifua kikuu,kwa hiyo zinahitajika nguvu za pamoja ili kuinusuru jamii kupata ugonjwa huo unaoongoza kupoteza maisha ya watu wengi hapa nchini.

Alisema,kifua kikuu ni hatari kwa kuwa ni rahisi sana kwa mtu mwenye ugonjwa huo ambaye bado hajaanzishiwa matibabu au kuacha kumeza dawa kuambukiza mtu mwingine kwa haraka zaidi kupitia mfumo wa hewa.

Dkt Kihongole alisema,kutokana na ukubwa wa tatizo hilo ndiyo maana serikali na wadau wengine imewekeza nguvu kubwa katika kupambana na ugonjwa huo ambapo matibabu yake utolewe bure katika zahanati,vituo vya afya na Hospital zote hapa nchini.

Alisema,serikali inatumia gharama kubwa katika kupambana na maradhi hayo  kwa kufanya kampeni za mara kwa mara za uelimishaji,uibuaji na uchunguzi ambazo zimesaidia kuwapata wagonjwa wa kifua kikuu ambao walibaki majumbani bila kupata tiba sahihi.

Ameagiza wagonjwa wa kifua kikuu waliokutwa katika kilinge hicho warudishwe Hospitali kuendelea na matibabu,na kuwataka waganga wa tiba asili kuacha  tabia ya kukumbatia wagonjwa wanaohitaji kupatiwa tiba za kitaalam.

Alisema,serikali inatambua shughuli za tiba asili zinazofanywa na waganga  hao,hata hivyo ni muhimu kunatoa tiba sahihi,kuacha udanganyifu kwa wateja wao, kuhakikisha wanafuata sheria na kuepuka kuchochea migogoro katika jamii.

Dkt Mkasange amewaagiza watendaji wa vijiji na kata,kuwakamata na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria waganga wa tiba asili wanaofanya kazi katika maeneo yao bila kufuata sheria  kwa kutokuwa na vibali vya serikali na kupiga ramli chonganishi.

Mtendaji wa kata ya Nandembo Zuber Ngoma,amewataka wananchi kujiridhisha  kwanza kabla ya kwenda kwa waganga wa tiba asili ambao baadhi wameonekana ni wababaishaji na matapeli wanaofanya kazi ili kujipatia kipato

Alisema,mara kwa mara serikali imekuwa ikitoa tahadhari kwa wananchi kuhusu hatari ya kukimbilia kwa waganga wanaotumia  shida na udhaifu wao kuwaibia,lakini changamoto kubwa ni imani potofu kwa jamii kwenye masuala ya asili.

Kwa upande wake Mganga wa tiba asili aliyekutwa na wagonjwa wa kifua kikuu katika kilinge chake Yasin Heja alijitetea kuwa,kwa sasa yuko kwenye mafunzo kwa vitendo ambapo anategemea kupata vibali mwezi Julai.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.