• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HOSPITALI ya wilaya ya Nyasa yaanza kutoa huduma za upasuaji

Imewekwa kuanzia tarehe: July 22nd, 2021

Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa,  leo imezindua rasmi na kuanza kutoa,  huduma za kulaza wagonjwa na Upasuaji wa Dharula, katika Hospitali ya Wilaya ya Nyasa iliyojengwa katika Kijiji cha Nangombo, Kata ya Kilosa Wilayani Hapa.

 Akizindua Huduma hizo Mkuu wa Wilaya ya Nyasa kanali Laban Thomas, amewata watumishi na wahudumu  wa Afya Wilayani hapa   kutoa huduma bora kwa Wazee, na wananchi na  wanaofika kupata huduma za matibabu katika Hospitali  ya Wilaya,  na kufanya kazi kwa bidii na  kufuata maadili ya kazi pamoja na viapo walivyokula.

Kanali laban amefafanua kuwa , mara baada ya kuanza kutoa huduma ya kulaza wagonjwa, na Upasuaji wa Dharula, ni mategemeo yake kuwa,  huduma  zitaboreshwa, na wananchi watapata huduma bora za afya, na Wazee watathaminiwa zaidi ili kuwaenzi, kwa kazi walizofanya kipindi wakiwa vijana za kulijenga Taifa la Tanzania.

Ameongeza kuwa atafurahi zaidi atakapoona Wazee wakipewa huduma bila kuwabagua, wala kuwasumbua, kwa kuwa nao wamechangia huduma nyingi za kulijenga Taifa letu, na kuwataka watumishi, kutoa Huduma kwa kufuata Sheria Taratibu na Kanuni kwa kuzingatia Viapo walipoapa.

“Ndugu wananchi wa Wilaya ya Nyasa na Watumishi wa Afya,  leo tukiwa tunafungua Huduma hizi za Kulaza wagonjwa, ninawataka, kuwapa Huduma bora wazee ambao nimewaalika leo, katika Zoezi hili  ili waone tunavyozindua huduma hizi, na ninawaagiza wazee hawa tunatakiwa kuwajali kwa kuwapa huduma bora, kwa kuwa nao walishafanya kazi za kulijenga Taifa .Aidha watumishi na Wahudumu wa Afya mnatakiwa kuwa na lugha nzuri kwa wagonjwa na wateja kwa kuwa wagonjwa wanahitaji hata faraja kutoka kwa Mtoa Huduma za Afya”. Amesema Kanali Thomas.

Awali akisoma Taarifa ya Uzinduzi wa Huduma za kulaza wagojwa na Upasuaji wa Dharula, katika Hospitali ya Wilaya ya Nyasa, Kaimu Mganga Mkuu Wilaya ya Nyasa Bw.Sixmund Maseti Ndunguru amesema, mara baada ya Uzinduzi huo, wamejipanga kuhakikisha kuwa, watatoa Huduma Bora kwa Wananchi wa Wilaya ya Nyasa wapatao 140,000, na wananchi wa wilaya jirani za Nchi ya Msumbiji, kupunguza Vifo vitokanavyo na Uzazi kwa kutoa Huduma Za dharula za upasuaji, kupunguza kasi ya magonjwa yasiyoambukiza kwa kutoa huduma elimu za afya na matibabu bora ya Ugonjwa wa kisukari , shinikizo la Damu, kansa kwa kuanzisha kliniki za kila wiki.

Amezitaja huduma zingine ni  Dawa muhimu na Vitenganishi vya maabara kwa kusimamia ukusanyaji wa mapato na kununua Dawa,Vifaatiba na Vitendanishi kwa wakati.

Kwa upande wao wananchi wa Wilaya ya Nyasa wameipongeza Serikali kwa Kuwatatulia changamoto ya Huduma za kulazwa wagonjwa na Upasuaji wa Dharula kwa kuwa awali Hudumahizi walikuwa wakisafiri Umbali Mrefu wa Kilometa 150 kupata matibabu katika hospitali ya Peramiho na songea.

Halmashauri ya Nyasa imekamilisha majengo saba ya awali ya Utawala, maabara, stoo ya dawa,mionzi,wodi ya wazazi,na jingo la kufulia, njia za kuunganisha majengo,Ujenzi ambao umegharimu Tsh Bilioni 2.291, na ujenzi wa Wodi ya Wanaume wanawake na watoto Unaendelea.Mradi huu wa Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya unatarajiwa kuwa na majengo 22 ambayo yatagharimu Tsh Bilioni 7.5.

Imeandaliwa na

 Netho C. Sichali

 Afisa Habari Nyasa Dc 0767417597.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.