• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HOSPITALI za Halmashauri 184 kufaidika na madaktari Bingwa

Imewekwa kuanzia tarehe: May 6th, 2024

Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI inaendesha kampeni maalum ya kusogeza huduma za afya za kibingwa katika hospitali za Halmashauri  184  Tanzania Bara.

Hayo yamesemwa na Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya Faraja Mgeni kwenye ufunguzi wa kambi ya matibabu ya kibingwa na ubingwa bobezi ya  Dkt.Samia  mkoani Ruvuma.

Madaktari bingwa 40  wameanza kutoa huduma za kibingwa katika Hospitali za Halmashauri zote nane mkoani Ruvuma,kuanzia Mei 6 hadi 10,2024

Mgeni amesema katika kipindi cha kuanzia Machi 2023 hadi kufikia Machi 2024  Wizara ya Afya kwa kushirikiana na TAMISEMI ilifanikiwa kuwajengea uwezo watoa huduma za afya Zaidi ya 4000  walioweza kutoa  huduma za kibingwa  kwa wananchi Zaidi ya 10,956.

“ ili kuimarisha huduma za afya kwa wananchi Wizara ya Afya na TAMISEMI inaendelea kuendesha kampeni maalum ya kusogeza huduma za afya za kibingwa katika hospitali za Halmashauri nchini,kampeni hii tunaianza leo Mei 6  na kukamilika Mei 28 mwaka huu na tutakuwa tumezifikia hospitali  184 zilizopo Tanzania bara’’,alisema.

Hata hivyo amesema katika Mkoa wa Ruvuma kampeni ya huduma za kibingwa inaanza Mei 6  na kukamilika Mei 10 mwaka huu na kwamba wananchi wanasogezewa huduma za kibingwa bobezi katika hospitali nane za  Halmashauri mkoani Ruvuma.

Ametoa rai kwa Viongozi katika ngazi zote mkoani Ruvuma kushirikiana na madaktari bingwa hao na kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi ili kupata huduma hizo za kibingwa.

Kwa upande wake mgeni rasmi kwenye ufunguzi huo,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed ambaye aliwakilishwa na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Gilbert Simiya, ameipongeza serikali kwa kutoa madaktari bingwa na bingwa bobezi wa Dkt.Samia Suluhu Hassan ambao wamefika kutoa huduma za kibingwa mkoani Ruvuma.

Kanali Abbas ametoa rai kwa madaktari hao kufanya kazi yao kwa ufanisi mkubwa kwa kuwa serikali imeboresha upatikanaji wa vifaa tiba na kwamba serikali inaendelea kuboresha huduma za afya mkoani Ruvuma.

“Katika Mkoa wa Ruvuma serikali imetoa shilingi bilioni 18.721  kutekeleza miradi ya afya ikiwemo ujenzi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa,ujenzi wa hospitali za Halmashauri,vituo vya afya na zahanati’’,alisisitiza Kanali Abbas.

Ameitaja miradi mingine iliyotekelezwa mkoani Ruvuma ni ukarabati wa hospitali kongwe ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru,Mbinga Mji na ujenzi wa majengo ya huduma za dharura (EMD) katika hospitali za Tunduru,Nyasa,Madaba na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dr.Louis Chomboko akizungumza kwenye ufunguzi huo amesema madaktari bingwa hao  wanatekeleza mpango kabambe wa huduma za mkoba nchini lengo likiwa ni kuboresha huduma za kibingwa karibu na wananchi katika ngazi ya Halmashauri.

Amewataja madaktari bingwa hao wanatoka katika hospitali za rufaa za mikoa,hospitali za Kanda,hospitali ya Taifa  na maalum na kwamba huduma za kibingwa zinazotolewa ni ubingwa  wa akinamama na uzazi,Watoto,upasuaji,magonjwa ya ndani,utoaji dawa za ganzi na usingizi.

Kampeni hii ya ina kauli mbiu ya madaktari bingwa wa Rais Samia tumekufikia karibu tukuhudumie ambayo imelenga kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma za kibingwa katika Halmashauri zao ili kuwapunguzia gharama za kusafiri umbali mrefu.

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBUNGE Kawawa aleta neema Namtumbo

    May 11, 2025
  • KIONGOZI Mwenge wa uhuru ashiriki upandaji miti Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru waweka jiwe la msingi shule ya amali Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru wazindua jengo la EMD Peramiho

    May 10, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.