• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HUWEZI kuzungumzia Uhuru wa Msumbiji bila kuitaja Tanzania

Imewekwa kuanzia tarehe: April 6th, 2021

Na Albano Midelo

NCHI ya Tanzania wakati huo ikiwa chini ya uongozi wa Rais wa Awamu ya Kwanza Hayati Mwl.Julius Nyerere ilishiriki kikamilifu kwenye harakati za ukombozi kusini mwa Afrika.

Nchi ya Msumbiji ni miongoni mwa nchi ambazo hazitaisahau Tanzania ilivyotoa mchango wake hadi kusababisha nchi hiyo kupata uhuru wake toka kwa wareno mwaka 1975.

Alfonso Kaidavid ni Mhifadhi kwenye makumbusho ya Taifa ya Msumbiji yaliyopo Matchedje Jimbo la Niassa, anasema serikali ya Msumbiji imeamua kuanzisha makumbusho katika eneo hilo kutokana na kufanyika mkutano wa pili mwaka 1968 uliosababisha nchi hiyo kupata uhuru wake.

Anasema mkutano wa kwanza wa harakati za kuikomboa Msumbiji ulifanyika jijini Dar es salaam nchini Tanzania mwaka 1962 ukiongozwa na Rais Julius Nyerere  wa Tanzania na viongozi waandamizi wa FRELIMO nchini Msumbiji ambao ni Edwardo Mondlane na Samora Machel.

Mhifadhi Kaidavid anasema Mkutano wa pili ulifanyika kwa siku tano katika eneo la Matchedje kuanzia Julai 20 hadi 25 mwaka 1968 na kwamba mkutano huo ulioongozwa viongozi waandamizi wakiwemo Rais Julius Nyerere wa Tanzania,Edwardo Mondlane na Samora Machel wa Msumbiji.

“Makumbusho haya tumeanzisha ili wanamsumbiji,watanzania na wageni wengine kutoka nchi mbalimbali waweze kujua ni namna gani nchi ya Msumbiji ilipambana katika kuikomboa nchi toka kwa wakoloni wareno ambao walitutawala kwa miaka mingi’’,anasisitiza Kaidavidi.

Anamtaja kiongozi wa FRELIMO hayati Edward Mondlane kwa kushirikiana na Samora Machel walipata mafunzo mbalimbali nje ya nchi ya Msumbiji namna ya kumfukuza mkoloni ili kuiacha Msumbiji huru.

Mhifadhi huyo anasema kabla ya kuamua kumwaga damu viongozi hao walijaribu kuzungumza na wareno ili wakubali kwa hiyari kutoa uhuru wa Msumbiji,hata hivyo ilishindikana ndipo waliamua kutumia njia ya bunduki.

Historia inaonesha kuwa wareno walifika nchini msumbiji mwaka 1498 na kwamba safari yao ilikuwa ni kwenda nchini India,hata hivyo waliamua kubaki Msumbiji,baada ya kubaini nchi hiyo ina utajiri mkubwa wa madini na meno ya tembo.

Akizungumzia vivutio vya utalii vilivyopo eneo hilo la kihistoria la Matchedje,Kaidavid anasema kwenye eneo hilo yamebakia masalia ya vibanda mbalimbali ambavyo viongozi wa kitaifa waliishi kwa siku tano kufanya mkutano wa pili  mwaka 1968 uliozaa uhuru wa Msumbiji.

Moja ya vivutio kwenye eneo hilo ni uwepo wa gogo  ambalo mwaka 1968 walikalia Rais Julius Nyerere wa Tanzania,Rais Edward Mondlane wa Msumbiji na Mkuu wa Majeshi alikuwa Samora Machel ambao walikaa kwenye gogo hilo kwa siku tano wakijadili namna ya kuikomboa nchi ya Msumbiji toka kwa wareno.

“Viongozi hao mwaka 1968 walijadili wakiwa wamekaa kwenye gogo hili ambalo hadi leo bado lipo likiwa vile vile bila kuoza,tumelihifadhi kama kumbukumbu muhimu kwenye harakati za ukombozi wa nchi ya Msumbiji’’,anasisitiza Mhifadhi huyo.

Maeneo mengine ambayo ni kivutio kwenye eneo hilo ni uwepo wa kibanda ambacho alilala kwa siku tano Rais wa Msumbiji Edwardo Mondlane mwaka 1968,pia kuna kibanda ambacho alilala Mkuu wa Majeshi Samora Machel kwa siku tano na kibanda ambacho walilala waandishi wa habari kwa siku tano.

Ukiachia harakati zilizoendelea nchini Msumbiji, eneo  la Masonya lililopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma nchini Tanzania lina utajiri wa utalii wa malikale na utambulisho wa Taifa,ingawa bado halifahamiki na wengi.

Eneo hilo lenye ukubwa wa ekari 100 lina vivutio adimu vya utalii wa malikale ikiwemo nyumba yenye namba A 10 ambayo walikuwa wanafikia na kuishi     Marais Hayati Julius Nyerere wa Tanzania na Hayati Samaro Machel wa    Msumbiji kuanzia 1966 wakati wa harakati za ukombozi Kusini mwa Afrika.

Mhifadhi wa  Makumbusho ya Taifa ya Majimaji Bartazar Nyamusya anasema viongozi hao pia wakiwa katika nyumba hiyo,walitumia jengo dogo maalum      lililopo jirani ya nyumba hiyo kama chumba cha mawasiliano yote na nchi    zilizokuwa katika harakati za ukombozi kusini mwa Afrika.

Kutoka nyumba ya viongozi hao hadi jengo dogo la mawasiliano,lilijengwa   handaki la chini kwa chini ambalo lipo hadi sasa lililokuwa linatumiwa na viongozi hao wa Tanzania na Msumbiji.

Eneo la malikale la Masonya lenye ukubwa wa ekari 100 lipo kilometa 12 kaskazini mwa mji wa Tunduru, eneo hili linatakiwa kuendelezwa kwa sababu linaweza kutoa mchango mkubwa katika nyanja za utalii,uchumi,elimu na utafiti.

Historia inaonesha kuwa Rais wa sasa wa Msumbiji Pilipe Nyusi amesoma shule ya msingi FRELIMO iliyokuwepo katika eneo la Masonya ambaye alifika hapo mwaka 1970 akiwa na umri wa  miaka nane.

Hata hivyo serikali hivi sasa inalitumia eneo la malikale la Masonya kwa shughuli za kielimu ambapo katika eneo hili imejengwa shule ya sekondari ya wasichana Masonya.

Kabla ya mwaka 1966,eneo la malikale la Masonya lilikuwa ni msitu ambapo katika mwaka huo ndipo serikali iliwapokea watu kutoka nchini Msumbiji na kuwakabidhi eneo hilo  katika kipindi chote cha kupigania uhuru nchini Msumbiji.

Nurdin Seleman ni Mwenyekiti wa kijiji cha Masonya  anasema kijiji hicho ilikuwa ni kambi ya wapigania uhuru wa  nchi ya Msumbiji na kwamba eneo hilo lina malikale mbalimbali zilizokuwa zinatumiwa na wananchi wa Msumbiji.

Anasema eneo hilo linatembelewa mara kwa mara na wananchi wa Msumbiji akiwemo Balozi wao  ambapo  serikali ya kijiji hicho inaendelea kuzitunza malikale hizo ambazo ni muhimu kwa vizazi vya sasa na vijavyo kwa maendeleo ya nchi zote mbili.

Erick Soko ni Afisa Elimu Msaidizi Makumbusho ya Taifa ya Majimaji anasema tangu mwaka 1966 walipokabidhiwa eneo hilo la Masonya,watu wa Msumbiji wanafanya ziara  kuona eneo waliloishi viongozi mashuhuri wa nchi hiyo, akiwemo Hayati Rais Samora Machel ambaye alifika mara kadhaa wakati wa harakati za kupigania uhuru.

“Katika kipindi cha miaka kumi kuanzia 1966,wanawake toka nchini Msumbiji wamekuwa wanaishi katika eneo la Masonya,Umoja wa Wanawake wa Msumbiji unaojulikana kwa OMM ulianzia Masonya mwaka 1973’’,anasema Soko.

Kulingana na Soko,Mwaka 1975 baada ya  uhuru wa Msumbiji kutangazwa ndipo kambi ya Masonya               ilivunjwa na wanamsumbiji walirejea katika nchi yao,tangu mwaka 1975 hadi mwaka 1989 eneo hili lilibaki bila matumizi.

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Julius Mtatiro anazitaja rasilimali adimu zilizopo katika eneo la malikale la Masonya kuwa ni majengo 13 ya FRELIMO na masalia ya kale ya nyumba za viongozi wa kitaifa ambao ni Hayati Julius Nyerere na Samora Machel.

Mtatiro anasema licha ya eneo hilo kuwa na majengo mengi yaliojengwa na watu wa Msumbiji na mengine ya serikali,bado kuna magofu na majengo mengi chakavu, hivyo ni muhimu eneo hilo kuboreshwa na kuhifadhiwa kwa malengo endelevu.

Kutokana na umuhimu wa eneo la Masonya katika harakati za ukombozi kusini mwa Afrika, Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Innocent Gashungwa ametembelea eneo hilo na kuagiza maeneo yote ya kihistoria yanalindwa na kutunzwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Gashungwa amelitaja eneo la Masonya kuwa limesheheni utajiri mkubwa wa historia ya Tanzania na namna Tanzania ilivyoshiriki katika harakati za ukombozi wa bara la Afrika.

Hata hivyo Gashongwa amefurahishwa na nyumba iliyotumiwa na Rais wa zamani wa Msumbiji hayati Samora Machel kati ya mwaka 1966 hadi nchi hiyo ilipopata uhuru mwaka 1975 na nyumba iliyokuwa inatumiwa na baba wa Taifa hayati Julius Nyerere.

 “Historia yote tajiri imezama katika kata ya Masonya,naziagiza Halmashauri zote nchini kutunza maeneo yote ya kihistoria,mimi  nitatembelea kila Halmashauri nchi nzima ili kuhakikisha maeneo yenye utajiri wa kihistoria yanatunzwa na kuhifadhiwa’’,alisisitiza.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Tunduru Mwajuma Abasi Nasombe  ameutaja urithi mwingine kwenye eneo la Masonya kuwa ni ukumbi wa semina aliokuwa anatumia Samora Machel kutoa mafunzo mbalimbali na majengo 11 ambayo kwa sasa ni madarasa ya wanafunzi wa sekondari ya wasichana Masonya.

Hata hivyo anasema mwaka 1975 baada ya nchi ya Msumbiji kupata uhuru wapigania uhuru hao walirudi  nchini kwao na kuanzia mwaka  1990 Halmashauri ya Tunduru iliamua kuanzisha shule ya sekondari ya wasichana Masonya ambayo hadi kufikia mwaka 2014 inachukua wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha sita.

Mawasiliano ya mwandishi simu 0784765917

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.