• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

IDARA ya Ardhi Mkoa wa Ruvuma yakusanya maduhuli ya serikali kwa asilimia 108

Imewekwa kuanzia tarehe: March 1st, 2021

KAIMU Kamishina wa Ardhi Msaidizi wa Mkoa wa Ruvuma Ildeforce Ndemela amesema Idara ya ardhi mkoani Ruvuma imekusanya maduhuli ya serikali kwa asilimia 108.

Akitoa taarifa kwa Naibu Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt.Angelina Mabula,Kaimu Kamishina wa ardhi amesema kiasi hicho cha fedha kimekusanywa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020.

Ndelema amesema serikali iliupangia Mkoa wa Ruvuma kukusanya maduhuli ya serikali ya shilingi 990,000 hadi kufikia Juni 30,2020 na kwamba Idara ilifanikiwa kukusanya shilingi bilioni 1,076,957,355.22 sawa na asilimia 108.

“Katika mwaka wa fedha wa 2020/2021 Idara ya Ardhi Mkoa wa Ruvuma imepangiwa lengo la kukusanya kiasi cha bilioni 4.6, hadi kufikia Februari Mkoa umekusanya shilingi milioni 740 sawa na asilimia 16,mikakati ya kuongeza makusanyo ya kodi ikiwemo ikiwemo kuandaa na kusambaza ankra za umiliki na Hati za madai ya kodi’’,alisema Ndemela.

Hata hivyo amesema Mkoa wa Ruvuma katika kipindi mwaka 2020/2021 umepangiwa lengo la kupima viwanja 16,550 na mashamba 104 ambapo hadi kufikia Februari 22,2021,viwanja 4,873 na mashamba matano yamepimwa katika maeneo ya mijini na vijiji kwa ajili ya matumizi mbalimbali.

Amesema Idara hiyo imepokea jumla ya michoro ya mipango miji 41  yenye jumla  ya viwanja 18,581 vya matumizi mbalimbali na kwamba zoezi la kurasimisha makazi holela linaendelea katika Halmashauri zote za Mkoa wa Ruvuma.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt.Angelina Mabula akizungumza baada ya kupokea taarifa hiyo amesema ukusanya maduhuri ya serikali kitaifa katika Wizara yake  imefikia asilimia 30 na Mkoa wa Ruvuma umefikia asilimia 16.

Kutokana na hali hiyo Naibu Waziri Mabula ameziagiza Halmashauri zote nchini kuongeza juhudi za ukusanyaji maduhuli ya serikali ili kufikia malengo waliojiwekea ikiwemo kukusanya madeni kwa kuzingatia sheria.

“Sheria ipo wazi,kifungu cha 50 kifungu kidogo cha kwanza cha sheria ya ardhi namba nne kinampa siku 14 tu mdaiwa anapokuwa amepewa Ilani,ndani ya siku 14 asipoweza kulipa,tunampeleka kwenye Baraza, kinachofuata ni yeye kulipa deni’’,alisisitiza.

Amesema ikishatolewa oda ya kutakiwa kulipa anatakiwa kulipa au kukamata mali zake na kuuzwa ili fedha ipatikane ambapo amewataka watendaji wa Ardhi waache kugeuza ukusanyaji maduhuli kuwa kufanyika kisiasa.

Dkt.Mabula amewaagiza maafisa ardhi kuongeza kasi ya kupima viwanja na mashamba na kwamba hatua kali zitachukuliwa kwa maafisa ardhi watakaoshindwa kutekeleza majukumu yao ikiwemo upangaji, upimaji, umilikishaji.uthamini,usajili wa hati,utatuzi wa migogoro ya ardhi na ukusanyaji wa maduhuli ya serikali.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Machi,Mosi,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.