• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

JAJI Mkuu atembelea mahakama ya Kigonsera Mbinga

Imewekwa kuanzia tarehe: March 4th, 2022

JAJI Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Juma amesema,Serikali itaendelea kujenga na kuzifanyia ukarabati mahakama kongwe hapa nchini ikiwamo mahakama ya mwanzo Kigonsera wilaya Mbinga mkoani Ruvuma ambayo imeanza kuchakaa.

Profesa Ibrahim Juma alisema,lengo ni kuwa na mazingira mazuri ya kazi kwa watumishi na sehemu nzuri ya kupata haki kwa watanzania na mkakati wa kuboresha huduma zake.

Alisema hayo jana,wakati akizungumza na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya ya Mbinga wakiongozwa na mkuu wa wilaya hiyo Aziza Mangosongo baada ya kutembelea jengo la mahakama ya mwanzo Kigonsera wilayani humo akiwa katika ziara ya kujionea hali halisi ya mahakama na kuzungumza na watumishi.

Aidha alisema,ujenzi na ukarabati unaoendelea kufanyika katika mikoa mbalimbali nchini utakuwa kipimo kwa mahakimu na watendaji wengine wa mahakama kwa sababu watakuwa na mahali salama na bora katika utekelezaji wa kazi zao.

Profesa Juma alisema,mkakati huo ulioanza kutekelezwa miaka mitano iliyopita tayari umeonesha mafanikio makubwa kwa kuwa mahakimu wanafanya kazi kwa kuzingatia maadili,wananchi wanapata huduma bora na kupungua kwa malalamiko.

Jaji Mkuu, amevutiwa na hatua ya wananchi kutumia vyombo vya sheria kama vile mahakama kudai haki zao badala ya kujichukulia sheria mkononi, hivyo kuwezesha wananchi kutumia muda wao kufanya shughuli za maendeleo.

Amewataka wananchi na wadau wengine wa mahakama wilayani humo, kutoa ushirikiano kwa mahakama ili kufanikisha malengo waliyojiwekea ya kumaliza usikilizaji wa mashauri yanayofikishwa mahakamani kwa wakati.

Kwa mujibu wa Jaji Mkuu, hayo yakitekelezwa serikali itapata muda mwingi wa kutekeleza miradi na shughuli mbalimbali za maendeleo, badala ya kujikita kushughulikia migogoro.

Mkuu wa wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma Aziza Mangosongo alisema, maboresho yaliyofanywa na mahakama katika kipindi cha miaka mitano yamesaidia kwa kiwango kikubwa kupunguza matukio ya uharifu katika wilaya hiyo kufuatia wananchi wengi kukimbia Mahakamani kutafuta na kudai haki zao.

Mangosongo ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya maadili ya Mahakama katika wilaya ya Mbinga, ameishukuru Mahakama kwa kuanza ujenzi wa mahakama ya mwanzo Matiri ambayo itakapokamilika itarahisisha usikilizaji mashauri kwa mahakimu.

Pia alisema,mahakama hiyo itasaidia sana kupunguza umbali mrefu wa wananchi kwenda maeneo mengine kusikiliza mashauri na kudai haki zao kupitia mhimili huo wa mahakama.

Mkuu wa wilaya alitaja changamoto kubwa katika wilaya hiyo ni masuala ya upelelezi wa kesi, lakini wanaendelea kuifanyia kazi ili kesi na mashauri yanayopelekwa mahakama yaweze kusikilizwa na kumalizika kwa wakati.

Mangosongo alisema, wananchi wengi wa Mbinga ni wakulima, kwa hiyo migogoro mingi inayotokea ni ya ardhi ambayo inafikishwa katika mabaraza ya kata na mara chache inafikishwa mahakamani.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Mbinga mjini Jonas Mbunda,ameipongeza Mahakama nchini kufanya maboresho makubwa ya miundombinu, jambo lililohamasisha wananchi wengi kwenda mahakamani kutafuta haki zao.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.