• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAKAMU wa Rais awaasa vijana kuepuka Biashara ya figo

Imewekwa kuanzia tarehe: July 22nd, 2023

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ametoa wito kwa watanzania hususani vijana kujiepusha na kutoa figo zao kwaajili ya kufanya biashara ili kuepuka madhara makubwa yanayoweza kujitokeza.

Makamu wa Rais amesema hayo leo tarehe 21 Julai 2023 akiwa ziarani mkoani Ruvuma mara baada ya kuzindua Jengo la kutolea huduma ya usafishaji figo lililopo katika hospitali ya Rufaa ya Mtakatifu Joseph – Peramiho. Amesema tabia hiyo inaweza kuhatarisha Maisha ya mwanadamu hususani pale figo iliobaki inaposhindwa kufanya kazi.

Aidha Makamu wa Rais ametoa rai kwa watanzania kujenga tabia ya kupima afya walau mara moja kwa mwaka ili kuepukana na hatari za maradhi kufikia hatua mbaya zaidi. Makamu wa Rais amesema ni vema kuachana na ulaji usiofaa, unywaji wa pombe kupitiliza pamoja na kuhimiza kufanya mazoezi kuepukana na hali hiyo.

Halikadhalika Makamu wa Rais amewataka viongozi na watalaam wa afya kuendelea kutoa elimu ya namna ugonjwa huo unavyopatikana ili kuwasaidia wananchi kuepukana nao.

Makamu wa Rais amesema ugonjwa wa Figo ni miongoni mwa magonjwa yanayoongoza kusababisha vifo vya watu wengi duniani ambapo nchini Tanzania inakadiriwa kuwa kwa kila Watanzania mia moja Watanzania saba wanasumbuliwa na ugonjwa sugu wa figo. Ameeleza kwamba asilimia kumi (10) ya wagonjwa sugu wa figo nchini wamefikia hatua ya mwisho ambayo inahitaji matibabu mbadala ya figo, yaani kusafishwa damu au kupandikizwa figo nyingine.

Makamu wa Rais ameongeza kwamba serikali inatekeleza afua mbalimbali zenye lengo la kuzuia na kudhibiti ugonjwa wa figo na magonjwa mengine yasiyoambukiza ambapo hadi sasa zaidi ya Madaktari bobezi wa figo 20 na zaidi ya Wauguzi bobezi 10 wamehitimu mafunzo na wanatoa huduma kwenye hospitali mbalimbali. Amesema kufikia mwisho wa mwezi Juni, 2023, serikali imefanikiwa kutoa huduma za kusafisha damu kwa wagonjwa takribani 3,500, paamoja na kupandikiza figo kwa wagonjwa 74 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na wagonjwa 33 katika Hospitali ya Kanda ya Kati ya Benjamin Mkapa, Dodoma.

Dkt. Mpango amepongeza Hospitali ya Rufaa ya Mtakatifu Joseph – Peramiho kwa kutoa huduma ya kusafisha figo ambayo itakua msaada kwa wananchi wa mkoa huo na maeneo ya Jirani.

Kwa Upande wake Mbunge wa Jimbo la Peramiho na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Jenista Mhagama ameishukuru serikali kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika eneo hilo katika sekta za Afya, Elimu na Miundombinu.

Waziri Mhagama amesema zaidi ya shilingi milioni 400 zimetolewa kwaajili ujenzi wa stendi ya kisasa katika Halmashauri hiyo pamoja na ujenzi wa zahanati katika vijiji 50.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.