• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

JUKWAA la kuimarisha uhifadhi wa ushoroba wa Selous Niassa Ruvuma lafunguliwa

Imewekwa kuanzia tarehe: December 11th, 2020


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amefungua Jukwaa la kuimarisha uhifadhi ushoroba wa Selous Niassa ambalo limefanyika kwa siku mbili  kwenye ukumbi wa Heritage Cottage mjini Songea.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Jukwaa hilo Mndeme amewaagiza wadau wa uhifadhi mkoani Ruvuma kuhakikisha kuwa ushoroba wa wanyamapori wa Selous Niassa unaimarika na kufikia malengo ya kunufaisha jamii za kizazi cha sasa na kijacho.

“Eneo la ushoroba wa Selous Niassa limebarikiwa kuwa na utajiri mkubwa wa rasilimali mbalimbali za mimea,wanyamapori,ndiyo maana Pori la Akiba la Selous limechaguliwa na UNESCO kuwa urithi wa dunia na kuanzishwa kwa Hifadhi ya Taifa ya Nyerere’’,alisema Mndeme.

Amesema ushoroba huo una makundi makubwa ya wanyamapori kama tembo,mbwamwitu,nyati,viboko na simba na kwamba ushoroba huo ni muhimu kwa hifadhi mbili za Tanzania na Msumbiji yaani Selous na Niassa.

Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa Mkoa,sekta ya utalii nchini inaingiza pesa nyingi za kigeni kwa kuwa inaleta wageni milioni 1.5 kwa mwaka na kwamba utalii pekee unachangia pato la Taifa kwa asilimia 17 na kutoa ajira kwa watanzania milioni mbili.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Uwanda wa Ruvuma wa Shirika la WWF Diana Shuma amesema jukwaa hilo la Mkoa ni la pili kufanyika likihusisha ushoroba wa Selous Niassa na kwamba kikao hicho kinawakutanisha wadau ili kujadili namna ya kuhifadhi ushoroba huo ambao upo katika hatari ya kutoweka.

Amesema ushoroba huo ni muhimu kwa Tanzania na Msumbiji kwa kuwa ni mapitio muhimu ya wanyamapori na unakabiliwa na changamto ya watu kufanya shughuli za kiuchumi ikiwemo kilimo na ufugaji.

“Lengo la kuanzisha jukwaa hili ni kuwaleta pamoja wadau  kujadili na kutengeneza mikakati ya kuhifadhi ushoroba huu wa Selous Niassa ambao una ukubwa wa hekta zaidi ya milioni  1.5’’,alisisitiza Shuma.

Fidel Kimario ni Mratibu Uhifadhi Wanyamapori na mapito ya wanyama Wizara ya Maliasili na Utalii amesema serikali imeandaa kanuni za kusimamia mapito ya wanyamapori ili kukabiliana na hatari ya kutoweka mapito ya wanyamapori.

Enock Msocha ni Kaimu Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Kanda ya Kusini Mashariki wa TAWA inayohusisha mikoa ya Lindi,Mtwara na Ruvuma,amesema wameongeza mbinu mbalimbali za kulilinda pori la Selous ikiwemo kuongeza doria katika maeneo yote wakati wote.

Hata hivyo amesema wanashirikiana na wananchi katika maeneo jirani ya hifadhi kufanya ulinzi na kufuatilia wanyama kwa karibu endapo wamevuka katika maeneo ya wananchi ili wananchi na wanyama waweze kuwa salama.

Imendikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Desemba 11,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.