• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KAMATI ya Bunge yakagua miradi ya maji ya bilioni 3.7 Nyasa

Imewekwa kuanzia tarehe: March 18th, 2024

Na Albano Midelo,Mbambabay

KAMATI ya Kadumu ya Bunge ya Maji na Mazingira ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mheshimiwa Jackson Kiswaga imeridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maji miwili inayogharimu shilingi bilioni 3.7 wilayani Nyasa mkoani Ruvuma.

Miradi iliyokaguliwa na Kamati hiyo ni mradi wa maji Ngumbo unaogharimu shilingi bilioni 2.5 na mradi wa maji Malungu Kata Tingi unaogharimu shilingi bilioni 1.2.

Akitoa taarifa ya miradi hiyo Meneja wa RUWASA Wilaya ya Nyasa Mhandisi Masudi Samila  ameutaja mradi wa maji Ngumbo ulianza kutekelezwa Novemba 2023 na unatarajia kukamilika Aprili 30 mwaka huu ambao utahudumia wakazi Zaidi ya 11,000.

Amezitaja kazi zinazotekelezwa katika mradi huo unaohudumia kata za Ngumbo na Liwundi ni ulazaji wa bomba la maji lenye urefu wa meta Zaidi ya 29,000,ujenzi wa vituo 30 vya kuchotea maji na ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita 200,000 na kwamba mradi  umefikia wastani wa asilimia 60.

Akizungumzia mradi wa maji Malungu,Meneja huyo wa RUWASA wilaya ya Nyasa amesema mradi huo unagharimu Zaidi ya shilingi bilioni 1.2  na kwamba utekelezaji wa mradi umefikia Zaidi ya asilimia 80 na unatarajia kuwanufaisha wakazi Zaidi ya 9,000.

Akizungumza baada ya kukagua miradi hiyo kwa nyakati tofauti,Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Marypricsa Mahundi  amesema awamu ya pili ya utekelezaji wa mradi huo itaendelea na kwamba mwezi ujao italetwa shilingi milioni 200 kuendelea kutekeleza mradi huo.

Amemwagiza Meneja wa RUWASA wilaya ya Nyasa kumsimamia Mkandarasi  kwa kushirikiana na viongozi wa vijiji ili mradi huo uweze kutekelezwa kwa wakati na kuanza kuwahudumia wananchi.

“Ni lazima wananchi tuwasogezee maji nyumbani ili waepukane na adha ya kuamka usiku kufuata maji,nani anataka kuamka usiku wa manane na kufuata maji,akinamama tutunze ndoa zetu,Meneja wa Wilaya haya ni maagizo tekeleza’’,alisisitiza Mhandisi Mahundi.

Amesema Rais Dkt.Samia Suluhu ameagiza kumtua mama ndoo kichwani ambapo amesema mama anatakiwa  asitembee umbali wa Zaidi ya meta 400  kufuata maji ili kumwezesha mama kushiriki katika shughuli za uzalishaji mali na kuongeza kipato.

Naye Mbunge wa Muleba Kaskazini Mheshimiwa Charles Mwijage amesema Rais Dkt.Samia ameokoa Maisha ya wanaume wa Wilaya ya Nyasa kwa kuwasogezea huduma ya maji.

Ametoa rai kwa wanaume kuhakikisha kuwa katika mradi wa maji awamu ya tatu wanaunganisha bomba hadi ndani ya nyumba ili akinamama waweze kupata maji ndani ya nyumba.

“Wanaume tunakufa sana,tatizo mojawapo linalosababisha tufe ni mama akienda kuchota maji mbali,wewe pressure inapanda juu kwa wivu,mama Samia kwa kuwaletea maji amewaokoa’’,alisisitiza Mwijage.

Naye Mbunge wa Jimbo la Nyasa Mhandisi Stella Manyanya  ameomba kuongezwa kwa vituo vya kuchotea maji viwe jirani Zaidi na wananchi.

Hata hivyo ameishukuru serikali kwa kutekeleza miradi hiyo ya maji ambayo inakwenda kumaliza changamoto ya maji  katika kata za Ngumbo, Liwundi na Tingi.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira Mheshimiwa Jackson Kiswaga amesema Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ametoa fedha za kutekeleza miradi ya maji Zaidi ya 1700 katika nchi nzima na kwamba katika Mkoa wa Ruvuma pekee serikali inatekeleza miradi ya maji 36 inayogharimu shilingi bilioni 66.

Ameahidi Kamati hiyo kushughulikia haraka changamoto mbalimbali za miradi ya maji walioikagua na kwamba lengo la serikali ni kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa asilimia 100 ambapo amesema watahakikisha fedha za wakandarasi zinatoka mapema ili waweze kukamilisha miradi hiyo.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.