• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KAMATI ya Siasa Mkoa wa Ruvuma ilivyoridhishwa na mradi wa bwalo Nyasa

Imewekwa kuanzia tarehe: June 30th, 2020

SERIKALI ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli, imetoa Sh milioni 150 kwa ajili ya utekelezaji wa ujenzi wa bwalo na jiko, katika shule ya Sekondari ya Kilumba, Kata ya Lumeme Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa Mkoani Ruvuma.

Akitoa taarifa ya mradi huo kwa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma, Kaimu Afisa Elimu Sekondari Halmashari ya Nyasa Oscar Elias amesema,  ujenzi wa Mradi huo umetekelezwa kwa kutumia Force account, ambao ulianza Septemba 20, 2019 na kukamilika Desemba 20 ,2019.

“Mradi umetoa ajira za muda kwa watu 60, ikiwa ni wanawake 16 na wanaume 44. Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa na wananchi wa Kata ya Lumeme, tunaishukuru Serikali ya CCM kwa kutekeleza kwa vitendo Ilani ya Chama cha Mapinduzi’’,alisema.

Akizungumza baada ya kukagua Mradi huo, Katibu wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Ruvuma Nuru Ngeleja, amesema Kamati ya Siasa ya CCM mkoa, imeridhishwa na utekelezaji wa mradi huo.

 Ngeleja amewaomba wananchi siku ya uchaguzi Mkuu  kujitokeza kwa wingi na kuwapigia kura Viongozi wa CCM, Kuanzia Rais, Wabunge na Madiwani ili kuwatia moyo ya kuendelea kuwatumikia, katika kipindi kingine cha miaka mitano.

Naye Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake  (UWT) wa Mkoa wa Ruvuma Kuruthumu Mhagama, amewapongeza wananchi wa Kata ya Lumeme, kwa kujenga bwalo, na bweni la Watoto wa kike katika Shule ya Sekondari Kilumba,ambapo amesema bweni litasaidia kupunguza mimba za utotoni.

Mhagama ameutaja Mkoa wa Ruvuma kuwa  ni miongoni mwa mikoa inayoongoza kwa mimba za utotoni, Hivyo amewaasa wazazi na walezi, kuwathibiti watoto wao ili kupunguza tatizo hilo na kuwawezesha watoto wa kike kutimiza ndoto zao.

Kwa upande wake Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM  Taifa, Musa Homera amesema ili kuonesha Shukrani  kwa, Rais John Magufuli,ameshauri kujitokeza kupiga kura nyingi za Ndiyo katika uchaguzi mkuu  Oktoba mwaka huu.

“Mimi nataka niwaambieni Shule, Hospitali na Majengo mengine ya Serikali yaliyojengwa Miaka 40 iliyopita, yanalingana na majengo yaliyojengwa kwa fedha za Serikali katika kipindi cha miaka mitano,  cha uongozi wa Rais Magufuli”, amesisitiza Homera.

Sera ya Elimu ya mwaka 2014 pamoja na ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015, inaipa kipaumbele sekta ya elimu na itahakikisha Serikali inasimamia sera ya elimu na mafunzo ya mwaka 2014.

Imeandaliwa na 

Albano Midelo na Netho Credo

Maafisa Habari Serikalini

Mbambabay

Juni 29,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.