• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KAMATI ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma yaagiza miradi yote ya maendeleo Tunduru kukamilika

Imewekwa kuanzia tarehe: July 3rd, 2020

KAMATI ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma imewaagiza watendaji na wataalam kusimamia na kuhakikisha miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao kukamilika ndani ya mkataba ili wananchi waweze kunufaika ma miradi hiyo.

Maagizo hayo yametolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma Odo Mwisho wakati kamati hiyo inakagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa nyakati tofauti wilayani  Tunduru.

Kamati haijaridhishwa na kutokamilika kwa asilimia 100 kwa miradi ya maji milonde kata ya Matemanga ambayo serikali imetoa zaidi ya shilingi milioni 215 ,kutekeleza mradi huo ambao umefikia asilimia 75,

Mradi mwingine ambao haujakamilika kwa asilimia 100 ni ujenzi wa bwalo la chakula katika shule ya sekondari Nandembo ambao serikali imetoa shilingi milioni 100 kutekeleza mradi huo.

Kamati ya Siasa ya CCM pia haijaridhishwa na kuchelewa kukamilika ujenzi wa bweni lenye uwezo wa kulaza wanafunzi 400  katika sekondari ya wasichana Masonya ambao serikali imetoa zaidi ya shilingi milioni 100 kutekeleza mradi huo.

Akizungumza kwa nyakati tofauti mara baada ya kukagua miradi hiyo,Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma ameagiza mradi wa maji milonde  kumalizika kabla ya mwezi Agosti mwaka huu  ili kuwaondolea kero ya maji wananchi.

“Hakuna sababu ya kushindwa kukamilisha mradi kwa sababu serikali imeleta fedha za kutosha,hadi sasa mmetumia milioni 44 kati ya milioni 215 zilizopo,huu ni uzembe,alaumiwe nani,DC fanyia kazi tupate taarifa ya mabadiliko kuanzia sasa’’,alisisitiza Mwisho.

Kuhusu bweni la shule ya sekondari ya wasichana Masonya Kamati hiyo imeagiza  kuhakikisha bweni linakamilika kwa asilimia 100 na wanafunzi wanaanza kulitumia ambapo ametaka huduma muhimu kama maji,umeme na vitanda na magodoro viwepo.

Amewatahadharisha watalaam kuchukua hatua haraka na kuhakikisha wanafanyakazi na kusimamia miradi kulingana na mikataba na maelekezo yanayotolewa na serikali ili kuwaondolea kero wananchi.

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Julius Mtatiro ameahidi kusimamia miradi hiyo ili iweze kukamilika kwa asilimia 100 na kuanza kutoa huduma kwa wananchi  ambao wanasubiri kwa hamu.

Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma ipo katika ziara ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Mkoa wa Ruvuma.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari wa Mkoa wa Ruvuma

Julai 4,2020

Tunduru

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.