• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KAMATI za maadili za mahakama zaimarishwa Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: February 11th, 2025

Tume ya Utumishi wa Mahakama imetoa mafunzo mkoani Ruvuma kwa wajumbe wa Kamati za Maadili ya Mahakama Ngazi ya Mkoa na Wilaya ya Songea yakiwa na lengo la kuongeza uelewa na ujuzi kwa viongozi na maafisa wa Mahakama waliopo katika kamati hizo.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati hiyo ngazi ya mkoa, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, akifungua mafunzo hayo ambayo yamefanyika katika ukumbi wa Mipango uliopo katika ofisi yake mjini Songea, amesema mafunzo hayo yanaongeza uelewa kwa viongozi na kuwakumbusha maafisa wa Mahakama namna wanavyotakiwa kuwahudumia wananchi.

Ameongeza kuwa kamati hizo zimetayarishwa kwa ajili ya kupokea malalamiko ya wananchi dhidi ya mahakimu ngazi ya mkoa na wilaya ambao watakuwa wamefanya makosa ya kimaadili, kutekeleza majukumu yao kwa uzembe au kukiuka maadili ya mahakimu pamoja na mwenendo mbaya katika jamii.

Naye Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Songea, Mhe. James Karayemaha, amesema mafunzo hayo ni muhimu pia ni dira ya kuwaonyesha wanapoelekea kwa kuwa yatawasaidia kujua namna ya kufanya kazi zao kwa weledi, uaminifu na namna ya kuwajibika.

Kwa upande wake Naibu Katibu Maadili na Nidhamu Tume ya Utumishi wa Mahakama, Alexia Mbuya, amesema changamoto kubwa ni wananchi kutojua uwepo wa kamati hizo hivyo wenyeviti wa kamati za maadili ya Mahakama kwa Mkoa na Wilaya wawasaidie kutoa Elimu kwa wananchi wanapokuwa katika mikutano ya hadhara ili wapate uelewa juu ya uwepo wa kamati hizo na majukumu wanayotekeleza.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma, Bi. Mary Makondo, amesema wao kama wajumbe wa kamati hizo katika ngazi ya mkoa na wilaya mafunzo hayo yanawapatia uelewa mkubwa na nuru kubwa kwa ajili ya kuwajibika.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.