• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KAMPENI ya umebima Kanda ya Kusini yazinduliwa Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: February 20th, 2023

BENKI ya NMB imezindua kwa mara ya tatu kampeni ya  umebima katika Kanda ya Kusini iliyolenga kutoa elimu ya uwekezaji  wa bima na umuhimu wake katika jamii.

Uzinduzi huo umefanyika katika Tawi la NMB Songea mkoani Ruvuma ambapo mgeni rasmi kwenye uzinduzi huo alikuwa ni Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mhe.Michael Mbano.

Akizungumza kabla ya kufanya uzinduzi huo ulioshirikisha  wadau mbalimbali wa NMB wakiwemo wafanyabiashara, kampuni mbalimbali za bima,watumishi wa umma na viongozi wa wajasiriamali wadogo(Machinga),Mstahiki Meya Mbano  ametoa rai kwa makundi mbalimbali kukata bima ili kukabiliana na majanga mbalimbali.

“Kila mfanyabiashara mdogo awe tayari kukata bima ya biashara yake,NMB wametuanzishia jambo ambalo ni muhimu sana kwa sababu majanga yanatokea muda wowote,hivyo wananchi wote watumie fursa ya bima ya NMB kuwa na uhakika wa Maisha katika biashara zao’’,alisisitiza Mbano.

Amesema wamachinga katika mji wa Songea na Mkoa wa Ruvuma kwa ujumla  baadhi yao wanamiliki biashara kubwa hivyo ili kulinda biashara zao wanatakiwa kukata bima ili kuwa na uhakika wa mitaji yao.

Kwa upande wake Meneja wa NMB Kanda ya Kusini Janeth Shango amesema kampeni ya umebima tayari imezinduliwa kitaifa mkoani Mbeya na hivi sasa uzinduzi  unfanyika katika ngazi ya  Kanda ambapo katika Kanda ya kusini yenye mikoa ya Mtwara,Lindi na Ruvuma uzinduzi umefanyika mjini Songea mkoani Ruvuma.

Amesema licha ya umuhimu wa bima katika Maisha ya kila siku,uchunguzi umebaini bado muitikio wa watu kuweka bima umekuwa mdogo hivyo NMB imeamua kuanzisha kampeni ya umebima ili idadi ya watanzania wanaoweka bima iweze kuongezeka walau kufikia asilimia 50 ifikapo mwaka 2029/2030.

Amesisitiza kuwa kampeni ya umebima inakwenda kutoa elimu ya bima kwa njia mbalimbali ili kuhakikisha watanzania wanaweka bima katika mali,afya au Maisha kwa ujumla ili kuongeza mchango wa sekta hiyo ndogo ya fedha kwenye pato la Taifa.

Ameitaja Benki ya NMB kuwa ndiyo Benki pekee nchini iliyozifikia wilaya zote nchini hivyo inaweza kusaidia upatikanaji wa huduma ya bima katika nchi nzima zikiwemo wilaya zote za Kanda ya Kusini.

“Bima ni kitu muhimu sana na imekuwa msaada mkubwa sana yanapotokea majanga mbalimbali,tujifunze kupitia majanga hayo yakiwemo ya moto hivyo tuendelee kuweka bima,ni muhimu idadi kubwa ya watanzania kujipatia bima’’,alisisitiza Shango.

Naye Mwenyekiti wa Klabu ya Wafanyabiashara Mkoa wa Ruvuma(NMB Bussines Club) Michael West  ametoa rai kwa wafanyabiashara wote kujiunga na bima ili kuchukua tahadhari dhidi ya majanga yanayotokana na Maisha.

Salum Masamaki ni Mwenyekiti wa Machinga Mkoa wa Ruvuma ameipongeza NMB kwa kutoa elimu ya kuweka bima kwenye masoko yote mjini Songea hali ambayo amesema itawawezesha wafanyabiashara wadogo kuweka bima  kuanzia ngazi ya chini.

Abed Nchimbi ni Mwenyekiti wa Bodaboda Mkoa wa Ruvuma na Salvatory Mangasila Mwenyekiti wa Bajaji Mkoa wa Ruvuma wameipongeza NMB kwa kuleta huduma ya bima ambayo itawawezesha wamiliki wa bodaboda  na bajaji ambao wamekopeshwa pikipiki hizo na NMB kuziwekea bima.

Kampeni ya umebima iliyozinduliwa mjini Songea inatarajiwa kufanyika kwa sita mtaa kwa mtaa, nyumba kwa nyumba na duka kwa duka ili kuhakikisha elimu ya umebima inawafikia  wananchi wote.

Imeandikwa na Albano Midelo Ruvuma

Februari 20.2023

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.