• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KAMPUNI YA JITEGEMEE yauza makaa ya mawe tani 500,000

Imewekwa kuanzia tarehe: January 8th, 2023

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Jitegemee Holdings, Emmanuela Kaganda ambayo inamiliki mgodi wa Makaa ya mawe katika kijiji cha Ntunduwaro Kata ya Ruanda Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma amesema shughuli za uzalishaji katika mgodi zilianza rasmi Mei 2021 na una uwezo wa kuzalisha tani 2,500 hadi 3,000 za makaa ya mawe kwa siku kwa mashine zilizopo kwa sasa.

Hata hivyo amesema hadi kufikia Desemba 2022, jumla ya dani 652,128.8 za makaa ya mawe zimevunwa.

“Hadi kufikia Mwezi Desemba 2022 kampuni imeshauza jumla ya tani 522,450.08 za makaa ya mawe kwa wateja wa ndani na nje ya nchi.


Amesema Kampuni imefanikiwa kusafirisha makaa ya mawe meli moja ya tani 22 kwenda nchini Congo DRC na mwezi huu wa Januari 2023 kampuni itasafirisha meli mbili za makaa ya mawe kwenda nje ya nchi. Meli moja ya tani 25,000 tayari ipo bandari ya Mtwara itaelekea Congo DRC na meli ya pili imeshafika nayo inapakia tani 55,000 za makaa kuelekea nchini Polland.”

Amesema kampuni yao imefanikiwa kuchangia shilingi bilioni 7.01 katika pato la Taifa, kati yake shilingi milioni 81.73 zimelipwa kwa halmashauri kupitia tozo na ushuru mbalimbali na Shilingi Milioni 292 ni kodi nyingine za serikali ikiwemo PAYE, kodi ya zuio na SDL.

“Kampuni imeshalipa Mrabaha jumla ya kiasi cha Shilingi Bilioni 3.59 na shilingi milioni 488 kama ada ya vibali vya kusafirisha mkaa nje ya nchi kuanzia Juni 2021 hadi Disemba 2022.”

Mkurugenzi huyo alikuwa anatoa taarifa ya mgodi huo kwa Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa alipotembelea na kukagua mgodi huo.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amekipongeza kikundi cha Mbalawala Women group kilichopo Ruanda, Wilaya ya Mbinga Mkoa wa Ruvuma ambacho kinajihusisha na utengenezaji wa mkaa wa kupikia kupitia makaa ya mawe na kwamba Serikali itaendelea kuwasaidia ili kuhakikisha wanaendelea na uzalishaji huo ambao ni muhimu katika utunzaji wa mazingira

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.