• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KANISA Tunduru latoa vifaa kituo cha afya Mchoteka

Imewekwa kuanzia tarehe: September 7th, 2023

KANISA la Upendo wa Kristo Masihi-Kiuma,limekabidhi vifaa tiba mbalimbali ambavyo gharama yake haijafahamika mara moja kwa kituo cha afya Mchoteka wilaya ya Tunduru ikiwa ni kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita kuboresha huduma za afya wilayani.

Mganga mfawidhi wa kituo hicho Dkt Theresia Rugemalila,amelishukuru kanisa la Upendo wa Kristo Masihi kwa msaada huo na kueleza kuwa,vifaa hivyo vitaboresha utoaji wa huduma za afya kwa wananchi wanaofika kupata matibabu kutoka kata ya Mchoteka na maeneo mengine ya wilaya ya Tunduru.

Dkt Rugemalila alisema, katika kituo hicho mahitaji halisi ya vitanda ni 60  na vilivyopo 27 tu upungufu vitanda 23,kwa  hiyo vitanda vilivyotolewa na kanisa vitaongeza nguvu hasa katika wodi ya akina mama na watoto ambako mahitaji yake ni makubwa.

Alisema,tangu kituo cha afya Mchoteka kilipopanuliwa kwa kujengwa majengo mapya,kimekuwa kimbilio  la watu wengi kutoka ndani na nje ya kata ya Mchoteka wanaokwenda kupata huduma za afya,kwa hiyo kupatikana kwa vitanda hivyo ni ukombozi mkubwa kwa kuwa vitasaidia kupunguza changamoto na mahitaji ya vitanda.

Amehakikishia Askofu wa kanisa hilo  Noel Mbawala kuwa,vifaa hivyo vitatunzwa na vitatumika kuokoa maisha ya Watanzania na kuwaomba wadau wengine kujitokeza kuisaidia  Serikali ya katika jitihada zake  katika kuboresha huduma za kijamii ikiwemo za afya

Alisema kuwa,serikali iko tayari kushirikiana na madhehebu ya dini na wadau mbalimbali katika kuhakikisha afya za wananchi zinakuwa salama,na kuongeza kuwa milango iko wazi kwa taasisi nyingine za dini zinazotaka kuunga mkono juhudi hizo za serikali ya awamu ya sita.

Kwa upande wake Askofu Mkuu wa kanisa la Upendo wa Kristo Masihi-Kiuma Noel Mbawala alisema,vifaa vilivyotolewa na kanisa hilo ni kutekeleza huduma ya kimwili,kuisaidia jamii na kuwawezesha madaktari na wauguzi kuhudumia wananchi.

Ametaja baadhi ya vifaa vilivyotolewa na kanisa hilo ni vitanda vya kulala watu wazima,vitanda vya kujifungulia na watoto,viti mwendo na kwamba huo ni mwendelezo wa kanisa hilo kusaidia huduma za kijamii katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Askofu Mbawala alisema,kanisa la Upendo wa Kristo Masihi-Kiuma linaamini kwamba ili mtu aweze kumtumikia Mungu ni lazima awe na afya njema,hivyo kupitia msaada wa vifaa tiba wagonjwa watahudumiwa vizuri na kurudi katika hali zao za kawaida kwa  kuendelea kumtumikia Mungu na kufanya shughuli zao za maendeleo.

Pia alisema,kanisa la Upendo wa Kristo Masihi limetoa magodoro 20 kwa wafungwa wa gereza la maji maji,wametoa mashine ya kudurufu karatasi(Printer)katika shule ya msingi Milonde na magodoro 20 katika shule ya Sekondari ya Matemanga.

Muuguzi kiongozi wa kituo hicho Baraka Mwakanjemba alisema,ili madaktari na wauguzi waweze kutekeleza majukumu yao vizuri lazima wawezeshwe vifaa,hivyo msaada huo utawaongezea morali na kuwatia moyo  katika utendaji wa kufanya kazi.

Alisema,kwa sasa kuna wauguzi wanne ambao wanalazimika kufanya kazi kwa masaa 24 ili wagonjwa wanaofika waweze kupata huduma bora na kuiomba serikali kuviongezea nguvu ya wafanyakazi na vifaa tiba vituo vya afya na zahanati zilizo maeneo ya pembezoni.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.