• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KAYA zaidi ya 4,000 Tunduru kunufaika na kilimo cha umwagiliaji

Imewekwa kuanzia tarehe: July 19th, 2024

ZAIDI ya kaya 4,000 katika Halmashauri ya wilaya Tunduru mkoani Ruvuma,zinatarajia kunufaika na fursa ya kilimo cha umwagiliaji kupitia utekelezaji wa mradi wa skimu ya umwagiliaji ya Nambarapi iliyopo kata ya Masonya wilayani humo.

Mradi huo unaotekelezwa na Serikali kupitia Tume ya Taifa ya umwagiliaji,utawanufaisha wakulima wanaolima mazao mbalimbali ikiwemo Mpunga,mahindi pamoja na mazao ya mboga mboga.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo Mhandisi wa umwagiliaji mkoa wa Ruvuma  Lusia Chaula alisema,mradi utatekelezwa kwa muda wa siku 560 kuanzia tarehe 15 Julai 2024 na utakamilika tarehe 31 Disemba 2025.

Chaula amezitaja gharama za mradi ni Sh.6,314,477,066.00 na utajengwa kwa kumtumia Mkandarasi kampuni ya M/S Company Ltd JV Otendo ambapo zaidi ya ekari 1,700 zimetengwa kutumika kwenye mradi huo.

Kwa mujibu wa Chaula, kazi zilizopangwa kutekelezwa  ni ujenzi wa banio na tuta,ujenzi wa mfereji mkuu mita 5,975,ujenzi wa mfereji wa upili mita 8,825,kujenga mfereji wa matupio,ujenzi wa barabara za mashamba,ujenzi wa vivusha maji na ofisi ya Mhandisi wa mradi

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya Tunduru Chiza Marando amesema,haijawahi kutokea katika wilaya hiyo kuwa na mradi wa umwagiliaji wenye thamani kubwa tangu wilaya ilipoanzishwa.

Marando amesema,mradi wa skimu ya umwagiliaji Nambarapi unakwenda kutoa uhakika wa chakula na kupatikana kwa ajira za muda kwa vijana wengi wanaotoka katika kata ya Masonya na wilaya ya Tunduru kwa ujumla.

“kupitia mradi huu tuna mhakikishia Mheshimiwa Rais  Dkt Samia Suluhu Hassan kwamba,wilaya ya Tunduru tutaendelea kuwa  na uwezo mkubwa wa kuzalisha na uhakika wa chakula ambacho kinaweza kutosheleza mahitaji ya wananchi wetu”alisema.

Mkuu wa wilaya ya Tunduru Simon Chacha,amemtaka mkandarasi kuhakikisha anatekeleza mradi huo haraka na  kwa viwango kama ilivyo kwenye makubaliano yaliyopo katika mkataba.

Chacha,amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa jitihada anazofanya za kuleta maendeleo  katika wilaya ya Tunduru ikiwemo kutoa zaidi ya Sh.bilioni 6.3 fedha ambazo zitatumika kutekeleza mradi huo wa umwagiliaji utakaowanufaisha wananchi wengi hususani wakulima wa wilaya ya Tunduru.




Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.