• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KICHWA cha Songea kurejeshwa nchini baada ya mwaka mmoja

Imewekwa kuanzia tarehe: February 27th, 2023

Wizara ya Maliasili na Utalii imeunda Kamati ya Kitaifa inayosimamia urejeshwaji wa malikale zilizo nje ya nchi,likiwemo fuvu la Jemedari wa Wangoni Nduna Songea Mbano ambalo limehifadhiwa nchini Ujerumani.

Jemedari wa wangoni Songea Mbano na wenzake mashujaa wa vita ya majimaji 66 walinyongwa na wajerumani mwaka 1906,ambapo wajerumani walikata kichwa cha Songea na kukipeleka nchini Ujerumani ambako kimehifadhiwa hadi sasa.

Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii ambaye pia ni Mkurugenzi Msaidizi wa  Idara ya Mambo ya Kale Dkt.Emanuel Bwasiri akizungumza kwenye  tamasha la kumbukizi ya mashujaa wa vita ya Majimaji mjini Songea,amesema Kamati ya kitaifa inaendelea vizuri kushughulikia suala hilo ili kuhakikisha malikale zote zilizo nje  zinarejeshwa nchini.

“Sisi kama Wizara tunaamini mipango yote iliyowekwa ikienda vizuri,tunatarajia baada   ya mwaka mmoja au miwili fuvu la Songea Mbano linaweza kurudishwa hapa nchini’’,alisisitiza.

Hata hivyo amesema fuvu la Songea Mbano litakaporudishwa mawasiliano yatafanyika kati ya wenye fuvu na serikali kuangalia namna fuvu hilo litakavyohifadhiwa hapa nchini.

Akizungumza kwenye kilele cha tamasha la kumbukizi la mashujaa wa vita ya Majimaji,mgeni rasmi Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii mheshimiwa Mary Masanja ameiagiza Kamati ya Kitaifa inayoshughulikia urejeshwaji wa malikale zilizopo nje ya nchi likiwemo fuvu la Songea,kuhakikisha wanatekeleza na kukamilisha kazi hiyo kwa haraka.

Amesisitiza kuwa serikali imedhamiria malikale hizo likiwemo fuvu la Songea Mbano zinarejeshwa hapa nchini na kuzifanya kuwa kumbukizi .

“Naomba kutoa taarifa rasmi kuwa miongoni mwa malikale zilizoshughulikiwa na kuhakikisha zinarejeshwa nchini ni Pamoja na fuvu la Songea Mbano ambaye ni miongoni mashujaa 67 wa vita ya Majimaji waliouwa kwa kunyongwa na wajerumani mwaka 1906’’,alisisitiza.

Amesema kumbukumbu za mashujaa wa vita ya majimaji zinawezesha kizazi cha sasa na kijacho kujifunza namna watanzania walivyojitolea maisha yao katika harakati za ukombozi dhidi ya wakoloni.

Naibu Waziri Masanja pia amekemea  vitendo viovu vinavyoendelea kujitokeza katika jamii  vinavyoharibu mila,utamaduni na desturi za mtanzania ambapo amewaasa wazazi na walezi kusimamia maadili mema kwa vijana wao.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas akitoa salamu za Mkoa kwenye kilele cha tamasha la kumbukizi la mashujaa wa Majimaji, amelitaja lengo la tamasha hilo kuwa ni kuwambuka mashujaa 67 waliouawa kikatili na wajerumani kwa kunyongwa Februari 27,1906 ambao walizikwa  katika eneo ambalo yamejengwa Makumbusho ya  Taifa ya Majimaji.

Amesisitiza kuwa tamasha hilo linasaidia kukuza utalii wa utamaduni na kurithisha mila na desturi za mtanzania kupitia matamasha ya utamaduni.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Dkt Noel Lwoga  amesema Makumbusho ya Taifa katika kuunga mkono juhudi za Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan  inalenga kuifanya jamii kuona umuhimu wa tamasha la Majimaji kwao na kuifanya ishiriki kikamilifu kutangaza mila,utamaduni na desturi zao.

Ameyataja malengo ya tamasha hilo kuwa ni kutambua mchango wa historia ya mapambano ya wananchi dhidi ya ukoloni na kuwaenzi wapiganaji wa vita ya majimaji,kutoa fursa kwa wadau kutembelea na kuona vivutio vya utalii vilivyopo kusini mwa Tanzania hususan mkoani Ruvuma na kuweka mkakati wa kuviendeleza.

Kaulimbiu ya tamasha la kumbukizi la mashujaa wa vita ya majimaji mwaka huu ni makumbusho yetu,urithi wetu kwa maendeleo ya utalii na uchumi.

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma

Februari 27,2023

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.