• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KISIMA cha maji chawakomboa wananchi Luhangarasi Nyasa

Imewekwa kuanzia tarehe: June 23rd, 2025


Wananchi wa Kijiji cha Luhangarasi, Kitongoji cha Punga katika Wilaya ya Nyasa, Mkoa wa Ruvuma wameipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapelekea mradi wa kisima cha maji safi na salama, hatua ambayo imeleta unafuu mkubwa katika maisha yao ya kila siku.

Mradi huo ni sehemu ya utekelezaji wa Programu ya Visima 900 inayosimamiwa na Wizara ya Maji kupitia Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), ambapo Wilaya ya Nyasa ni miongoni mwa wilaya zinazofaidika. 

Kisima hicho cha Punga tayari kimekamilika na huduma ya maji imeanza kutolewa rasmi kwa wananchi.

Akizungumza kuhusu utekelezaji wa mradi huo, Kaimu Meneja wa RUWASA Wilaya ya Nyasa, Mhandisi Evart alisema mradi huo unahudumia wakazi wapatao 3,498 wa eneo hilo. 

Alisema kazi iliyofanyika ni pamoja na uchimbaji wa kisima, ununuzi na ufungaji wa pampu, tanki lenye ujazo wa lita 10,000, vifaa vya ujenzi pamoja na ufungaji wa mfumo wa sola ambapo Jumla ya Shilingi milioni 79.5 zilitumika kutekeleza mradi huo.

Mbunge wa Jimbo la Nyasa, Mhandisi Stella Manyanya, alizindua rasmi mradi huo na kueleza kuwa kwa muda mrefu wananchi wa Kitongoji cha Punga walikuwa wakikabiliwa na changamoto kubwa ya maji, hivyo kukamilika kwa mradi huo ni ukombozi mkubwa kwao hasa kina mama na watoto waliokuwa wakitembea umbali mrefu kutafuta huduma hiyo muhimu.

Mradi huu wa maji safi na salama si tu umepunguza adha ya upatikanaji wa huduma ya maji, bali pia ni ushahidi wa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kuboresha maisha ya Watanzania waishio vijijini


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RUVUMA yang'aa kwenye ramani ya maendeleo;uwekezaji wa Trilioni 1.8 wageuza maisha ya wananchi

    June 23, 2025
  • KISIMA cha maji chawakomboa wananchi Luhangarasi Nyasa

    June 23, 2025
  • KITUO cha polisi cha kisasa chafunguliwa Namtumbo kwa gharama ya milioni 798

    June 22, 2025
  • JENISTA MHAGAMA akabidhi mashine na ng'ombe Peramiho

    June 22, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.