• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KITUO cha Afya Mapera Mbinga chafanikiwa kufanya upasuaji kwa mafanikio makubwa

Imewekwa kuanzia tarehe: July 5th, 2021

Kituo cha Afya Mapera kilichopo Kata ya Mapera, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kimeanza rasmi kutoa huduma ya upasuaji ikiwa ni mara ya kwanza kwa kituo hicho kutoa huduma hiyo.

Huduma hiyo imeanza kutolewa leo Julai Mosi 2021 ambapo jumla ya akina mama wajawazito watatu wamefanyiwa upasuaji na kufanikiwa kujifungua salama, wawili kati yao wakijifungua watoto wa kike na mmoja akijifungua mtoto wa kiume.

Akizungumzia kuhusu upasuaji huo, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, Dkt. Louis Chomboko, ambaye pia ameongoza zoezi hilo amesema upasuaji huo umefanyika kwa mafanikio makubwa na kwamba akinamama wote watatu waliopata huduma hiyo, na watoto waliozaliwa hali zao zinaendelea vizuri.

"Zoezi la leo ni mwanzo tu, ndio tumeanza kutoa huduma hii ambayo itakua endelevu na ambayo itasaidia wananchi wa maeneo haya na maeneo ya jirani kutolazimika kwenda mbali kwa ajili ya kufuata huduma ya upasuaji kwani kwa sasa huduma hiyo inatolewa hapa Mapera". Amesema Dkt. Chomboko.

Aidha, ameongeza kuwa mkakati na mpango wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga ni kuendelea kuboresha na kupanua zaidi huduma za afya katika kituo hicho ikiwemo huduma za  Meno na Radiolojia (X-Ray na Ultrasound) ambazo zitaanza kutolewa hivi karibuni.

Ikumbukwe kuwa mwaka 2019 Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga ilipokea fedha shilingi milioni 400 kutoka Serikali Kuu kwa ajili ya ujenzi wa majengo yanayopewa kipaumbelele ili kuimarisha huduma ya Afya ya Msingi na utoaji wa huduma za rufaa kwenye Kituo cha Afya Mapera, ujenzi ambao ulianza Agosti 2019 na kukamilika Februari 2020.

Miundombinu iliyokamilika kutokana na matumizi ya fedha hizo ni pamoja na Jengo la Upasuaji (Theatre), Jengo la Maabara (Laboratory), Nyumba ya mtumishi inayojitegemea (staff house), Jengo la kufulia nguo (Laundry) na Jengo la Wazazi (Martenity).

Miundombinu mingine ni jengo la kuhifadhia maiti (Mortuary), Kichomeo Taka (Incinerator), Shimo la Kutupia Kondo la nyuma (placenta pit) na Mfumo wa kuvunia maji ya mvua ambayo kukamilika kwa ujenzi huu kumesaidia kuhudumia wakazi zaidi ya 64,000 waliopo Tarafa ya Hagati na meneo mengine ya jirani.

Imeandikwa na
Salum Said,
Afisa Habari, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.