• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KIWA NJA cha Ndege Songea kufungua fursa za uwekezaji na utalii

Imewekwa kuanzia tarehe: April 6th, 2023

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas akiwa ameongozana na Kamati ya Ulinzi na Usalama, amekagua mradi wa ukarabati wa kiwanja cha ndege cha Songea ambacho serikali imetoa  zaidi ya shilingi bilioni 37 kutekeleza mradi huo.

Akizungumza mara baada ya kukagua mradi huo,Mkuu  wa Mkoa ameishukuru serikali ya Awamu ya sita kwa kuhakikisha kuwa Tanzania na Mkoa wa Ruvuma unaendelea kufunguka katika Nyanja mbalimbali za usafiri ukiwemo usafiri wa anga.

“Leo nimefika hapa katika uwanja wa ndege wa Songea kukagua kazi ambazo zimekuwa zinaendelea za kukarabati uwanja huu,ikiwemo kuurefusha uwanja na miumbombinu ambayo sasa imewezesha   kuongeza  ratiba  ya safari za ndege kutoka mara mbili kwa wiki hadi mara tatu’’,alisema RC  Thomas.

Ametoa rai kwa wananchi mkoani Ruvuma ,mikoa jirani na Nyanda za Juu Kusini kuutumia uwanja wa ndege wa Songea ambao sasa upo tayari kutumika kusafiri  kwa haraka ndani ya Tanzania na kuelekea maeneo mengine duniani.

Mkuu wa Mkoa anayakaribisha mashirika mengine ambayo yanaliona soko la usafiri wa anga la Kusini kupitia Songea wafike kwa sababu uwanja wa ndege upo salama na kwamba kiu ya wananchi wa Ruvuma ni kuhakikisha kuwa biashara zinafanyika kwa haraka zaidi ndani na nje ya nchi kupitia usafiri wa anga.

Hata hivyo Kanali Thomas amesema kufunguliwa kwa uwanja wa ndege wa Songea,kuna fungua  fursa za uwekezaji na  utalii,kwa sababu Mkoa una vivutio  vya kila aina likiwemo ziwa Nyasa,Hifadhi ya Taifa ya Nyerere,Mto Ruvuma,milima ya Livingstone na maeneo mengi yenye utalii wa kihistoria na kiutamaduni.

Kwa upande wake Meneja wa Ndege wa Songea Jordan Mchame amesema mara baada ya serikali kukarabati kiwanja cha ndege,idadi ya abiria inazidi kuongezeka ambapo ndege ya Bombadier yenye uwezo wa kubeba abiari 76 hivi sasa inabeba abiria kati ya 65 hadi 74.

“Hali hiyo inaonesha kwamba kuna abiria wengi wanaosafiri kwa ndege kwa kutumia  uwanja wa ndege wa Songea,usafiri wa anga ni wa haraka na salama kuliko aina nyingine zote za usafiri,kadri idadi ya abiria inavyoongezeka tunatarajia hata gharama za nauli zitapungua’’,alisisitiza Mchami.

Hata hivyo amesema kabla ya ATCL kuanza kutoa huduma,nauli ya ndege binafsi kutoka Songea hadi Dar es salaam kwenda pekee ilikuwa kati ya shilingi 500,000 hadi 600,000 ambapo  hivi sasa kupitia ATCL nauli kwenda ni shilingi 250,000 ,ambapo kwenda na kurudi ni shilingi 375,000 tu.

Kiwanja cha ndege wa Songea ni miongoni mwa viwanja  bora vya ndege Tanzania ambacho kilijengwa kati ya mwaka 1974 hadi 1980 na kiliwekewa lami hivyo kuwa na uwezo wa kutua ndege majira yote masika na kiangazi.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.