• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KIWANJA cha Ndege cha Songea kilivyoufungua ukanda wa Kusini

Imewekwa kuanzia tarehe: March 10th, 2025

Katika kona ya kusini mwa Tanzania, Kiwanja cha Ndege cha Songea kinasimama kama lango kuu la anga kwa wakazi wa mkoa wa Ruvuma na maeneo jirani.

 Kiwanja cha Ndege cha Songea kilichojengwa eneo la Ruhuwiko Manispaa ya Songea ni mojawapo ya viwanja 58 vinavyosimamiwa na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), kiwanja hiki kimepitia mabadiliko makubwa katika safari yake ya maendeleo, hasa katika mwaka wa fedha 2023/2024 ambapo serikali ilitoa Zaidi ya shilingi bilioni 37 kuboresha kiwanja hiki.

Historia na Uboreshaji wa Miundombinu

Katika juhudi za kuboresha huduma, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kupitia TAA ilitenga fedha kwa ajili ya kukarabati na kubadilisha jengo lililokuwa likitumiwa na mkandarasi mshauri kuwa jengo la abiria la kisasa.

Mradi huu unajumuisha ukarabati wa ukumbi wa kuondokea abiria wenye uwezo wa kuhudumia abiria 145 kwa wakati mmoja, ukumbi wa kuwasili abiria, pamoja na ujenzi wa maegesho ya magari ya kisasa.

Mbali na hayo, kiwanja hiki pia kimeboresha mifumo ya usalama kwa kusimika kamera za ulinzi, mfumo wa matangazo wa umma (PA system), pamoja na mifumo ya mawasiliano ya mtandao ili kuhakikisha huduma bora kwa wasafiri na wahudumu wa kiwanja.

Huduma za Ndege: Safari za Ratiba na Dharura

Ingawa safari za anga zinaendelea kukua, kwa sasa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) ndilo pekee linalotoa huduma za ratiba katika kiwanja hiki.

Shirika hilo linafanya safari mara tatu kwa wiki, yaani Jumatatu, Jumatano, na Ijumaa. Hii ni hatua kubwa kwa wakazi wa Songea na mkoa mzima wa Ruvuma ambao sasa wanapata huduma za anga kwa uhakika zaidi.

Ukuaji wa Idadi ya Miruko ya Ndege na Abiria

Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, kiwanja hiki kimeshuhudia ongezeko kubwa la miruko ya ndege na idadi ya abiria. Mnamo mwaka 2019, miruko ya ndege ilikuwa 304, lakini hadi mwaka 2023, idadi hiyo iliongezeka hadi miruko 468.

 Vilevile, idadi ya abiria imepanda kwa kasi kubwa kutoka abiria 2,025 mwaka 2019 hadi kufikia abiria 56,884 kufikia Juni 2024. Ongezeko hili linaashiria maendeleo ya uchumi na usafiri wa anga katika eneo hili.

Maendeleo yanayoshuhudiwa katika Kiwanja cha Ndege cha Songea yanatoa matumaini mapya kwa wakazi wa Ruvuma na Tanzania kwa ujumla.

Ukarabati wa miundombinu na ongezeko la safari za ndege ni dalili za ukuaji wa sekta ya anga na umuhimu wake katika kukuza uchumi wa ndani.

Kwa mwelekeo huu, Songea inazidi kujiimarisha kama kitovu cha usafiri wa anga kusini mwa Tanzania.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.